Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Golliwogg's Cake-walk. Allegro giusto
Ratiba Podcast
2023.04.18 Askofu Mkuu Tanzania: Jude Thaddeus ameadhimisha Misa kwa 'UKWATAKA' Jimbo Kuu Katoliki Dar Es Salaam,Tanzania 2023.04.18 Askofu Mkuu Tanzania: Jude Thaddeus ameadhimisha Misa kwa 'UKWATAKA' Jimbo Kuu Katoliki Dar Es Salaam,Tanzania 

Askofu Mkuu Ruwai’ch kwa UKWAKATA:msiwe na mpasuko na mitafaruku

Kutoa shuhuda wa dhati,kuacha mpasuko,mitafaruku,utumbuizaji kanisani,kugeuza nyimbo kuwa biashara na mengine ndio ushauri na maonyo aliyoelekeza UKWAKATA,Jimbo Kuu Katoliki Dar Es,Salaamu,wakati wa Misa Takatifu iliyofanyika Parokia ya Salasala Jumatatu ya Pasaka 2023.

Na Angella Rwezaula, - Vatican.

Askofu Mkuu Jude Thaddeus Ruwai’ch wa Jimbo Kuu Katoliki Dar Es Salaam, hivi karibuni, Jumatatu ya Pasaka, tarehe 10 Aprili 2023 aliongoza misa Takatifu kwa ajili ya Umoja wa Kwaya Katoliki Tanzania(UKWAKATA), katika Parokia ya Salasala, Jimbo Kuu katoliki la Dar Es Salaam, kwa kuongozwa na Injili ya siku iliyosoma na ambayo ilikuwa inaelezea ushuhuda wa wanawake walioacha kaburi kwa haraka wakiwa na hofu na furaha kubwa wakakimbia kuwatangazia wanafunzi wa Yesu Ufuko wake ili waende Galilaya ndipo wangemwona Yesu Mfufuka. Askofu Mkuu Ruwai’ch alisisitiza juu ya kutoa ushuhuda kama wanakwaya ambao walifika kumshuhudia Kristo kwa sababu  ni jambo jema. Tendo hilo ni kuonesha wazi kwamba wao ni Wakristo wengine, na ambao wanapaswa kufanana na Kristo zaidi.

Askofu Mkuu Jude Thaddeus wakati wa maadhimisho ya misa 10 Aprili 2023
Askofu Mkuu Jude Thaddeus wakati wa maadhimisho ya misa 10 Aprili 2023

“Tunapojiruhusu tusakamwe na dhambi tunaharibu ule wasifu wa kuwa kama Kristo, tunavuruga maana ya ubatizo tuliopewa, ambao ulitufanya tuzaliwe upya, tuwe watoto wa Mungu, tuwe ndugu zake Kristo na ambaye alitufanya tuwe hekalu au makao ya Roho Mtakatifu”, Alisisitiza Askofu Mkuu. Askofu Mkuu Taddeus, kwa njia hiyo aliwaomba wajifunze kutoka katika udhaifu wa Petro, lakini udhaifu huo uwasaidie kushinda udhaifu wao na kwa kila mmoja. Kwa  upande mwingine aliwaomba wajifunze kuwa na uthubutu na ufuasi amini wa kama wale wanawake waliomfuata Yesu mpaka wakaona anakufa  msalabani. Lakini pia hawakuishia hapo, bali walihangaika pia  na kutaka kuutunza mwili wake baada ya kuzikwa. Askofu Mkuu  Ruwai’ch pamoja na  kuwatia moyo,  na kuwasifu, alipenda pia kutoa angalisho ambalo ni muhimu katika utume wao kwa sababu  wamepewa kipaji cha kutangaza Injili kwa njia ya kwaya.

Wanawakaya kutoka parokia mbali mbali Jimbo Kuu Dar Es Salaam, Tanzania
Wanawakaya kutoka parokia mbali mbali Jimbo Kuu Dar Es Salaam, Tanzania

Kwa kufanya hivyo aliomba wakumbuke maneno ya Mtakatifu Agostino, ambaye alikuwa Askofu wa Hippo,  Barani la Afrika (alizaliwa tarehe 13 Novemba 354 mjini Thagaste katika mkoa wa Numidia, leo hii mji huo unaitwa Souk Ahras nchini Algeria)  ambaye alifundisha  kwamba: “anayeimba vizuri anasali mara mbili”. Askofu Mkuu awali ya yote  aliwaomba watafiti moyo na kuwaliza maswali kwamba kuimba kwao kunahusisha sauti zao au kuhusisha mioyo, dhamiri na nafsi zao?  Aliwashauri kwa hiyo wapende kuimba vizuri na waimbe vizuri kutoka katika kina cha mioyo yao na roho zao. Wanapoimba waimbe, wakitangaza kile wanachoamini, waimbe na wakishi kile wanacho kiamini, waimbe wakishuhudia kile wanachoamini, wakiimbe wakishangilia kile wanachokiamini.

Misa ya UKWATAKA Dar Es Salaam iliudhuriwa na waamini wengi sana
Misa ya UKWATAKA Dar Es Salaam iliudhuriwa na waamini wengi sana

Kwa kuongezea Askofu Mkuu Ruwai’ch alisema na ili hilo liweze kufanyika, lazima kazi ifanyike ya kutafiti moyo. Kwa udadisi zaidi, Askofu Mkuu Taddeus aliuliza  maswali wanakwaya  waliokuwa hapo na wakiwa wa kweli kunyosha mikono: “Ni wangapi wangeweza kupata komunia siku hiyo? Baada ya kunyosha mikono aliendelea tena kuuliza: “Je ni wangapi ambao wasingeweza kukomunika siku hiyo? Na  wakati huo huo akiwaomba wasiogope kunyosha kwa sababu hasingewauliza maswali maana wao  wanajua wenyewe  sababu gani zinawafanya hivyo. Lakini kwa kujibu alisema hicho “ndicho  kinachowafanya pia washindwe kuimba na kusali mara mbili; kushinda kuimba kutoka katika kina ya moyo, nafsi zao, na kushindwa kumtukuza na kumtukia Mungu kwa uwepo wao wote”.

Ametoa ushauri  Askofu Mkuu wa Dar es Salaam Tanzania kwa wanakwaya
Ametoa ushauri Askofu Mkuu wa Dar es Salaam Tanzania kwa wanakwaya

Askofu Mkuu Jimbo katoliki la Dar Es Salaam vile vile aliuliza swali la pili kwa sababu hapo walikuwapo wanawaka kutoka parokia mbali mbali kwamba: “Ni kwaya ngapi ambazo zimekwisha gubikwa na mgogoro? Je huo mgogoro umesababishwa na nini? Je huo mgogoro unamtumika Mungu? Kwa kuongezea alisema: “kwa sababu zipo kwaya ambazo zimeingia mgororo na paroko, mgogoro na wanakwaya wenzao, zipo kwaya ambazo zimeingia mgogoro na kamati tendaji, zipo kwaya ambazo zimeingia migogoro mingine mengi”. Kwa hiyo alibainisha kuwa  wanapoingia kwenye migororo  wao “ni watu wa mipasuko, sio watu wa amani, sio wacha Mungu, sio wajumbe wa habari njema tena ni wajumbe wa mitafaruku”. Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar Es Salaam aliwaomba  wanakwaya wajitafiti, wajitathimini na daima wahakikishe kwamba chembe chembe za migogoro, chembe chembe za mitafaruku zisiingie kati yao. Aliwasihi wakatae hiyo mipasuko na mitafaruku, na wakatae chochote kile kinacholeta mivutano kati yao na waamini wenzao, kati yao na wachungaji wao, kati yao na kazi zao tendaji. Kama wajumbe wa Injili, basi wao wawe wajumbe wa amani.

Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar Es Salaam wakati wa maadhimisho ya Misa kwa Ukwakata
Askofu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar Es Salaam wakati wa maadhimisho ya Misa kwa Ukwakata

Askofu Mkuu  na Mfansiskani Mkapuchini na mkuu wa Kanisa la Dar Es Salaam,  vile vile hakukosa pia kutoa angalisho jingine kwa UKWAKATA  kwamba  wao kama wanakwaya kazi yao msingi sio kutumbuiza. Kwa sababu kuna kuishawishi cha kutumbuiza. Kutokana na hilo aliomba wawasaidia wanapokuwa kwenye ibada, ili wasali nao na pamoja nao lakini sio kutumbuiza. “Msitutumbuize, tuhamasisheni tusali, tuhamasisheni tumsifu Mungu, tuhamasisheni tumtukuze Mungu na tujenge Ufalme wa Mungu kati yetu”, alisistiza Askofu Mkuu Ruaich. Pamoja na hayo, alisema kuwa  wasikubali kuwa watumbuizaji na hivyo pia akawaomba wakwepe mtego wa kugeuza kwaya kuwa ni chombo cha kibiashara.

UKWAKATA
UKWAKATA

Kwa kutoa mfano, Askofu Mkuu Taddeus alisema: “siku hizi tunapata soko za kanda na vyombo mbali mbali vinavyobeba muziki, ni vizuri na, mkitengeneza album mbali mbali mtaziuza na zitatufurahisha, lakini lengo la kwanza lisiwe la kufanya biashara. Lengo lenu la kwanza kwa hiyo ni kutangaza Injili”, alisisitiza Askofu Mkuu. Kwa kuhitimisha alipenda kuwarudisha tena kwenye neno la Mtume Petro lisemalo: “Nasi tu mashahidi wake”, na  aliomba umati mzima kanisani urudie kifungu hicho na  kuwatakia heri za Pasaka.

MAHUBIRI KWA UKWAKATA
18 Aprili 2023, 17:04
Prev
March 2025
SuMoTuWeThFrSa
      1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031     
Next
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930