Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Presto
Ratiba Podcast
WYD Fiumicino, Roma wanaandaa kuondoka kwa vijana katika hija huko Lisbon. WYD Fiumicino, Roma wanaandaa kuondoka kwa vijana katika hija huko Lisbon.  (ANSA)

WYD Lisbon:Vijana 65,000 wa Italia watakuwa katika siku ya vijana

Wanaowasindikiza ni maaskofu 106 pamoja na mapadre,watawa wa kike na kiume waelimishaji na wahuishaji.Katika mji mkuu wa Ureno,ujumbe wa bluu utaonekana unaowakilishwa na majombo 180 ya Italia.

Na Angella Rwezaula,-Vatican.

Katika taarifa kutoka Ofisi ya Kitaifa ya mawasiliano ya kijamii, ya Baraza la Maaskofu Italia (CEI) kuhusiana na Tukio la Siku ya vijana duniani ambalo linakaribia, imebainisha kwamba ushiriki wa vijana ni 65,000 wa Italia ambao wanaondoka kuelekea katika  Siku ya Vijana Duniani huko Lisbon, iliyopangwa kuanzia tarehe 1 hadi 6 Agosti 2023. Hao watasindikizwa na maaskofu 106 pamoja na mapadre, watawa wa kike na kiume  , waelimishaji na wahuishaji. Katika mji mkuu wa Ureno, ujumbe wa bluu utaonekana ambao unawakilishwa na majimbo 180  utakuwa na nyumba ya Italia ,“Casa Italia”, kama sehemu yake ya kumbukumbu, mahali pa kupata habari na nyenzo, kutatua matatizo, na pia kukutana, kutumia muda pamoja na kubadilishana uzoefu,  hata kwa kukaa nyumbani au kwenye mitandao ya kijamii shukrani kwa WIFI  bila malipo.

Vijana wako tayari katika tukio hilo muhimu kwa ajili yao.
Vijana wako tayari katika tukio hilo muhimu kwa ajili yao.

Sekretarieti ya Huduma ya Kitaifa ya Kitengo cha kichungaji cha  Vijana ambayo itatoa msaada kwa wale wanaowasindikiza  na viongozi wa vikundi, ofisi ya Ubalozi na kituo cha matibabu. Pia watakuwepo wafanyakazi wa Ofisi ya Kitaifa ya Mawasiliano ya Kijamii ya Baraza la Maaskofu Katoliki Italia (CEI )ambao watatoa ripoti kuhusu Siku ya vijana (WYD) kwenye tovuti https://gmg.chiesacattolica.it/ na  watasaidia wanahabari wa Italia na waendeshaji vyombo vya habari waliotumwa  huko Lisbon. Kukaribishwa kutahakikishwa na watu wa kujitolea wapatao thelathini kutoka Italia yote.

Siku ya vijana duniani Lisbon 1-6 Agosti 2023
Siku ya vijana duniani Lisbon 1-6 Agosti 2023

Makao makuu ya rangi Tatu kama Bendera ya Italia  huko Lisbon yatazinduliwa na Askofu Giuseppe Baturi, Askofu Mkuu wa Cagliari na Katibu Mkuu wa Baraza la maaskofu Italia (CEI), Dominika tarehe 30 Julai saa 6 Mchaza  (saa za Ureno). Ikilinganishwa na mpango rasmi wa WYD, vijana wa  Italia watashiriki kuanzia tarehe 2 hadi 4 Agosti katika katekesi zitakazofanywa na Maaskofu katika maeneo ya malazi ya mahujaji. Tarehe 2 Agosti, saa nane mchana (saa za Ureno), Passeio Maritimo de Algés itakuwa mwenyeji wa “Siku Kuu ya Waitalia,  ambao utakuwa ni muda wa kushiriki na kutafakari na utatangazwa mbashara na  Tv2000 kuanzia  saa 3.00 usiku  (saa za Kiitaliano). Uzoefu wa timu ya bluu utarekodiwa na Avvenire, Tv2000, InBlu2000 na Shirika la habari Sir na huduma za kujitolea, maalum na za moja kwa moja. Taarifa na sasisho kwa wakati halisi pia kwenye mitandao ya kijamii ya Kitengo cha  Vijana na Baraza la  Maaskofu wa Italia.

“Ushiriki wa majimbo  ambayo yamekuwa yakijiandaa kwa uteuzi huu kwa miezi kadhaa, na ushiriki mkubwa wa vijana unaelezea Kanisa hai na changa kuliko sisi kufikiria. Lisbon itakuwa na uzoefu fulani kwa sababu kadhaa: kwanza kabisa, kizazi ambacho kinashiriki ndani yake, kutokana na masuala ya umri, hakijawahi kupata kitu sawa lakini kinatokana na mateso ya janga; zaidi ya hayo, ni mara ya kwanza kwa mkutano wa dunia wa vijana kufanyika katika bara ambako kuna vita”. Alisema Padre  Michele Falabretti, mkuu wa Huduma ya Kichungaji Kitaifa ya  Vijana ya Baraza la Maaskofu Italia ( CEI). Kwa kuongezea  “Kila WYD ni maabara kubwa: tamaduni tofauti, lugha, asili hufungua moyo kwa uelewa wa kuwepo yenyewe. Toleo hili, hasa, litatumika pia kukuza uaminifu kwa wengine, ufahamu kwamba tunategemeana, kwamba tunahitaji kutambuana kama ndugu na kwamba inafaa kujihusisha. Na kufanya hivyo, kama Papa Francisko ametukumbusha, kwa fumbo hilo la safari ambayo daima iko karibu na wengine na sio peke yetu”.

26 Julai 2023, 15:48
Prev
March 2025
SuMoTuWeThFrSa
      1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031     
Next
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930