Tafuta

Hija ya Kitume ya Papa Francisko Malta:Amefika Malta katika ziara ya 36 ya kitume!

Papa Francisko amefika kwa Ndege ya Italia kisiwani Malta mara baada ya saa moja na nusu ya safari.Wakati wa kuwasalimia waandishi wa habari amewaeleza hata nia ya kwenda Kiev.Hata hivyo shauku ni kubwa katika kisiwa hiki kwa maasa 48 tu.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Upepo mkali wa Bahari ya Mediterania ulikaribisha kuwasili kwa 'Papa Frangisku' hili ndilo jina lake katika lugha ya ndani  ya kisiwa cha Malta, katika visiwa vilivyochaguliwa na Baba Mtakatifu kama marudio ya safari ya 36 ya kitume ya Papa. Hija hii ni fupi lakini nzuri ya chini ya masaa arobaini na nane hivi, kama Papa mwenyewe alivyothibitisha katika ndege, ambapo, akiwasalimu waandishi wa habari walioandamana naye,alisema kwamba wazo la safari ya kwenda Kiev ni pendekezo kwenye meza yake.

Papa akizungumza na waandishi wa habari katika ndege
Papa akizungumza na waandishi wa habari katika ndege
Papa akisalimiwa waandishi wa habari waliosindikizana nao kwenye ndege
Papa akisalimiwa waandishi wa habari waliosindikizana nao kwenye ndege

Akiwa Vella, Papa Francisko ametembea katika zulia jekundu hadi Sebule ya Rais na wenyeji wake  na Sebule ya Waziri Mkuu wa Mchi. Muda mfupi baadaye alipelekwa na gari hadi Ikulu huko Valletta.

Ziara ya Kitume ya 36 Kimataifa ya Baba Mtakatifu huko Malta na Gozo 2-3 Aprili
Papa akiwa na Rais na Mke wake wakitembea katika zulia jekundu katika uwanja wa ndege mara baada ya kufika
Papa akiwa na Rais na Mke wake wakitembea katika zulia jekundu katika uwanja wa ndege mara baada ya kufika
Umati wa Watu wa Malta wakimkaribisha Papa
Umati wa Watu wa Malta wakimkaribisha Papa

Umati mkubwa waliimba, huku wakipiga kelele na vigelegele: “Papa Francis, Papa Francis!” Ziara ya heshima imefanyika kwa rais, ambaye, pamoja na mke wake, waliongozana na Papa kwenye Chumba cha mapokezi ambapo wabadilishana zawadi. Pia hapa kumefanyika mkutano mfupi wa faragha na Waziri Mkuu Robert Abela na familia yake, ambapo mwisho wake mkutano umepangwa, katika Chumba cha Baraza Kuu, na mamlaka na wanadiplomasia. Hapo itakuwa ni hotuba ya kwanza.

Papa akitia saini kwenye kitabu cha wageni huko Ikulu akiwa na Rais na Mke wake
Papa akitia saini kwenye kitabu cha wageni huko Ikulu akiwa na Rais na Mke wake
Papa akiwa na Rais na Mke wake
Papa akiwa na Rais na Mke wake
02 April 2022, 11:47