Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
MASIFU YA JIONI KWA KILATINI
Ratiba Podcast

Papa amemkumbuka Papa Benedikto XVI:anamshukuru Mungu kwa ukarimu wake!

Kwa hisia nzuri tunamkumbuka mtu mwema,mkarimu sana.Ni Mungu pekee ndiye anayejua thamani na nguvu ya maombezi yake,ya sadaka zake zilizotolewa kwa ajili ya manufaa ya Kanisa.Ndivyo Papa amemkumbuka “mpendwa Papa Mstaafu aliyeaga dunia leo,katika mahubiri ya Masifu ya Jioni kwa ajili ya siku kuu ya Bikira Mama wa Mungu katika Kanisa la Mtakatifu Petro.

Na Angella Rwezaula; – Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko ameadhimisha Masifu ya Kwanza ya Siku Kuu ya Bikira Maria Mama Mtakatifu wa Mungu katika Kanisa kuu la Mtakatifu Petro Vatican na kwa kuhitimisha kwa wimbo wa mwisho wa Te Deum wa  shukrani, Jumamosi jioni tarehe 31 Desemba 2022, siku ambayo amefariki Papa Mstaafu Benedikto XVI na katika mahubiri yake amemkumbuka “kwa hisia  kali na shukrani kwa Mwenyezi Mungu ya kumtoa zawadi kwa Kanisa na kwa ulimwengu, kwa mema yote yaliyofanywa, na zaidi ya yote kwa ushuhuda wake wa imani na sala, hasa katika miaka hii ya mwisho ya maisha yake ya kustaafu”. Mada iliyoongoza mahubiri ya Papa Fransisko ni fadhila ya wema na ukarimu  ambao si  wema wa Kikristo peke lakini pia kiraia ambao unaweza kufanya ulimwengu kuwa wa kindugu zaidi. Papa Francisko kwa maana hiyo akianza mahibiri yake amesema “Alizaliwa na mwanamke( Gal4,4). Ilipotimia wakati, Mungu alijifanya mtu  hakuja ulimwenguni kwa kuanguka kutoka juu mbinguni; alizaliwa na Maria. Hakuzaliwa katika mwanamke bali na mwanamke. Ni jambo tofauti kwani ina maana ya kusema kuwa Mungu alitaka kuchukua mwili kutoka kwake. Hakumtumia, lakini aliomwomba ile ndio ya kukubali.  Na hapo akaanza pole pole mchakato wa mimba ya ubinadamu usio na dhambi na uliojaa neema na ukweli, uliojaa upendo na uaminifu. Ubinadamu mzuri, mwema na wa kweli, sura na mfano wa Mungu, lakini wa mwili wetu ulitolewa kwa Maria; hakuna kama yeye aliwahi kusema ndio, kwa uhuru, kwa kujitoa bure, katika heshima na katika upendo.

Masifu ya Jiioni tarehe 31 Desemba 2022
Masifu ya Jiioni tarehe 31 Desemba 2022

Hii ni njia ambayo alichagua Mungu ili kuingia ulimwenguni na katika historia, na huo ndio mtindo. Na mtindo huo ni muhimu kwa namna yake alivyokuja. Umama wa kimungu wa Maria, umama wa ubikira, umama unaozaa, ni njia ainayoonesha heshima kubwa sana ya Mungu kwa ajili ya uhuru wetu. Yeye ambaye alituumba pasipo sisi, hawezi kutuokoa pasipo sisi ( Mt. Agostino, CLXIX, 13).) Mtindo wake wa kuja kutuokoa ni njia ambayo hata hivyo inatualika kuifuata, kwa ajili ya kuendelea pamoja Naye ili kusuka ubinadamu mpya, huru, na uliopatanishwa. Ni mtindo,na namna ya kuhusiana kwetu ambako kunatokana na fadhila nyingi za kibinadamu, za kuishi vema na kwa hadhi. Moja ya fadhila hizi ni ukarimu, kama mtindo wa maisha ambayo yanasaidia udugu na urafiki kijamii (Fratelli tutti 222-224). Baba Mtakatifu Francisko amebaninisha kuwa: “Kwa kuzungumzia juu ya ukarimu, katika wakati huu wazo kuu lilikwenda kwa “Mpendwa Papa Mstaafu Benedikto XVI ambaye leo asubuhi ametuacha. Kwa hisia kali tunamkumbuka kwa namna hiyo mtu mkuu na mkarimu. Na tunahisi katika moyo wa shukrani kubwa: shukrani kwa Mungu kwa kumtoa kwa ajili ya Kanisa na Ulimwengu; shukrani kwake, kwa wema wote alioutimiza, hasa kwa ushuhuda  wa imani na sala, hasa katika miaka ya mwisho wa maisha ya ndani. Ni Mungu peke yake anajua thamani na nguvu yake ya maombi na sadaka zake alizotoa kwa wema wa Kanisa”, Papa amethibitisha.

Masifu ya Jioni 31 Desemba 2022
Masifu ya Jioni 31 Desemba 2022

Baba Mtakatifu Francisko ameongeza kusema: “ Jioni hii ninataka kupendekeza ukarimu hata kama fadhila za kiraia, kwa kufikiria kwa namna ya pekee Jimbo letu la Roma”. Ukrimu ni mktadha muhimu wa utamaduni wa majadiliano, na majadiliano ni muhimu kwa ajili ya kuishi kwa amani, kama ndugu ambao si kwamba wanaelewana daima, ni kawaida, lakini ambao wanazungumza, wanasikilizana na wanatafuta kuelewana na kuingilia kati pamoja. Ni kufikiria tu kwamba ulimwengu ungekuwaje bila mazungumzo ya uvumilivu kwa watu wengine wakarimu  ambao walijaribu kuunganisha familia na jumuiya. Majadiliano yasioisha na jasiri hayafanyi habari kama migongano na migogoro, licha ya hayo yanasaidia kifaragha ulimwengu kuishi vizuri (Ft 198). Kwa hiyo ukarimu ni sehemu ya majadiliano. Sio suala la sheria na wala masuala ya kauli mbiu, mtindo wa uhakika… hainamanishi hili kwa kuzungumzia ukarimu. Kinyume chake ni fadhila za kurudisha na kufanyia matendo kila siku, kwa kwenda kinyume na fikira za mitindo ya kisasa, na kufanya jamii yetu kuwa ya kibinadamu. Kiukweli, Baba Mtakatifu Francisko amebainisha kuwa, madhara ya ubinafsi, kuhusu hutumiaji hovyo, huko machoni pa wote. Na madhara makubwa zaidi ni kwamba wengine, ambao wanaotuzunguka, wanaeleweka kama vizingiti vya utulivu wetu, na katika usalama wetu. Wengine, wanatusumbua, wanatupotezea muda wetu  na rasilimali za kuweza kufanya kile tunachotaka na kupenda. Jamii ya kibinafsi na inayotumia hovyo inakuwa na uchokozi, kwa sababu wengine ni washindani wa kushindana nao (FT 222). Pamoja na  jamii hizi zetu na hata katika hali ngumu zaidi, kuna watu ambao wanajionesha kama vile kuna uwezekano wa kuchagua ukarimu na hivyo mtindo wao wa maisha unageuka kuwa mtindo huo katikati ya giza.

Masifu ya Jioni tarehe 31 Desemba 2022
Masifu ya Jioni tarehe 31 Desemba 2022

Baba Mtakatifu Francisko katika tafakari yake  ameendelea kukazia kwamba Mtakatifu Paulo katika Barua yake kwa Wagalatia iliyosomwa katika liturujia hiyo, alizungumzia juu ya matunda ya Roho Mtakatifu,na kati ya matunda hayo anataja kwa neno la Kigiri chrestotes (taz  5,22). Kwa hiyo ukarimu ndio tunaweza kuutegemea kama mtindo wa wema, ambao unasaidia na kufariji wengine kwa kuzuia kila dharau na ugumu. Mtindo ambao unaweza kutumika kwa jirani kwa kufanya kuwa makini bila kumkwaza kwa maneno au kwa ishara, kwa kutafuta kupunguza uzito wa mwingine, kwa kumtia moyo, kumpa nguvu, kumfariji na kamwe kutomdhalilisha, au kumdharau(Ft 223). Ukarimu ni dawa dhidi ya baadhi ya magonjwa ya jamii yetu: dhidi ya ukatili, ambao kwa bahati mbaya unaweza kuharibu, kama vile sumu katika moyo na kuweka sumu katika uhusiano; dhidi ya wasiwasi na haraka nyingi ambazo zinatufanya kujifikiria binafsi na kuwabagua wengine. (Ft 224). Magonjwa haya, ya maisha yetu ya kila siku, yanatufanya kuwa washambuliaji na wasio na uwezo wa kuomba ruhusa, au hata samahani, au hata kusema neno dogo tu la “Asante”.  Na ndivyo hivyo inapotokea katika njia, au dukani, au katika ofisi tunapokutana na mtu mkarimu tunabaki tumeshangaa, na utafikiri ni muujiza mdogo, kwa sababu kuwa ukarimu kwa sasa sio jambo la kawaida. Lakini shukrani kwa Mungu wapo bado watu wakarimu, ambao wanajua kuweka pembeni wasi wasi wao ili kutoa umakini kwa wengine, kutoa zawadi ya tabasamu, neno la kutia moyo, kwa kusikiliza mwingine mwenye kuhitaji msaada na hata kujieleza vya kutosha( FT).

Mahubiri ya Papa Francisko tarehe 31 Desemba 2022
Mahubiri ya Papa Francisko tarehe 31 Desemba 2022

Baba Mtakatifu Francisko kwa maana hiyo  Papa amekazia kuwa kurudisha ukarimu kama fadhila binafsi na ya kiraia, inaweza kusaidia na sio kidogo kuboresha maisha katika familia, katika jumuiya na katika miji. Kwa maana hiyo mwaka huu mpya wa Jiji la Roma. Amependa kutoa matashi mema kwa wote ambao wanaishi humo kukua katika fadhila hiyo ya ukarimu. Uzoefu unafundisha kuwa ukarimu ikiwa unakuwa mtindo mmoja wa maisha, unaweza kuunda kuishi vema, kwa kuweka ubinadamu ule uhusiano wa kijamii na kuyeyusha ushambuliaji na sintofahamu.  Papa akitazama picha iliyokuwa imepambwa kwenye Kanisa, Papa: “Ameomba kutazama picha ya Mama Bikira Maria. Leo na kesho,  katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, tunaweza kumuheshimu katika picha ya Mama wa Karmine wa Avigliano huko Potenza”. Tusidharau fumbo la Mama wa Mungu! Tuache tushangazwe na uchaguzi wa Mungu, ambao ungeonekana katika ulimwengu kama mitindo elfu ikionesha ukuu wake na kinyume chake alipendelea kufanyika mwili kwa uhuru kamili katika umbu la Maria, alipendelea kuumbika kwa miezi tisa kama mtoto na hatimaye kuzaliwa kwake, kuzaliwa na mwanamke. Hatuwezi kwa haraka kukaa na kutafakari yote  kwa sababu ni suala muhimu sana la fumbo la wokovu. Kwa maana hiyo ni kutazama katika kujifunza mtindo wa Mungu, heshima yake isiyo na kikomo kwa namna ya kusema ukarimu wake  kwa sababu katika umama wa Kimungu wa Bikira Maria kuna njiia kwa ajili ya ulimwengu wa kibinadamu zaidi.

Mahubiri ya Papa kwa Masifu ya Jioni 31 Des 2023
31 Desemba 2022, 20:15
Prev
March 2025
SuMoTuWeThFrSa
      1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031     
Next
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930