Papa Francisko:tuombe Mama Maria wakati wa shida yuko karibu nasi!
Na Angella Rwezaula, - Vatican.
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 23 Agosti 2023, amefanya katekesi katekesi yake katika Ukumbi wa Paulo VI kwa waamini na mahujaji kutoka sehemu mbali mbali za dunia. Baba Mtakatifu Francisko kwa hiyo katika mwendelezo wa mfululizo wa katekesi zinazohusu ari ya kutangaza Injili ametazama bara Bara la Amerika kuhusu ushuhuda wa Mtakatifu Juan Diego wa Mexico, mjumbe wa Bikira wa Guadalupe, mfano ambao Baba Mtakatifu amependekeza kwa waamini ili kumzungumza na Maria, Mama, ambaye upendeleo wake na kama wa Mungu, unawahusu wadogo na wanyonge. Kwa njia hiyo Papa akianza katekesi yake amesema “Katika safari yetu ya kugundua tena shauku ya kutangaza Injili, ari ya kitume, tukiona jinsi ari hiyo ya kitume,na shauku hiyo ya kutangaza Injili ilivyokua katika historia ya Kanisa katika mchakato wa safar ya kuona Amerika. Hapa uinjilishaji una chanzo cha kudumu huko Guadalupe.
Ni chemchemi hai. Wamexico wana furaha! Bila shaka, Injili ilikuwa tayari imefika kabla ya tokeo hilo, lakini kwa bahati mbaya pia ilikuwa imeambatana na mambo ya kidunia. Badala ya njia ya kiutamaduni, njia ya haraka ya kupandikiza na kuweka vielelezo vilivyowekwa awali Ulaya kwa mfano ilichukuliwa mara nyingi sana, ikikosa heshima kwa watu wa kiasilia. Kwa upande mwingine, Bikira wa Guadalupe alionekana akiwa amevaa nguo za wenyeji, alizungumza lugha yao, alikaribisha na kupenda utamaduni wa mahali hapo: Maria ni Mama na chini ya vazi lake kila mtoto anapata nafasi. Ndani ya Maria, Mungu alifanyika mwili na, kwa njia ya Maria, anaendelea kufanyika mwili katika maisha ya watu. Hakika, Mama Yetu humtangaza Mungu kwa lugha inayofaa zaidi, yaani, lugha ya mama.
Na kwetu sisi pia Mama Yetu anazungumza nasi kwa lugha yake ya asili, ile tunayoielewa vizuri. Injili inasambazwa katika lugha mama. Baba Mtakatifu ameongza kusema “Na ningependa kusema shukrani kwa mama na bibi wengi ambao hupitisha kwa watoto wao na wajukuu: imani hupita na maisha, kwa sababu hii mama na bibi ni watangazaji wa kwanza. Papa ameomba wapigiwe makofi mama na mabibi!.... Na Injili inawasilishwa, kama Maria anavyoonesha, kwa urahisi: Mama yetu daima huchagua kirahisi, kwenye kilima kile cha Tepeyac huko Mexic, kama huko Lourdes na Fatima: akizungumza nao, anazungumza na kila mmoja, kwa lugha inayofaa kwa wote. kwa lugha inayoeleweka, kama ile ya Yesu. Kwa njia hiyo Papa ameomba kujikita kutazama ushuhuda wa Mtakatifu Juan Diego, ambaye ni mjumbe,, wa kiasili aliyepokea ufunuo wa Maria: mjumbe wa Mama Yetu wa Guadalupe.
Juan alikuwa mtu mnyenyekevu, Mhindi wa watu: macho ya Mungu yalikaa juu yake, ambaye alipenda kufanya maajabu kupitia wadogo. Juan Diego alikuwa tayari ameanza kujongelea imani akiwa mtu mzima na kuoa. Mnamo Desemba 1531, alikuwa na umri wa miaka 55 hivi. Wakati yuko njiani, alimwona Mama wa Mungu juu ya kilima, ambaye alimwita kwa upole, na jinsi gani alimwita Mama, “Mwanangu mdogo mpendwa Juanito”(Nican Mopohua, 23). Kisha alimtuma kwa Askofu ili aombe kujenga hekalu pale pale ilipoonekana. Juan Diego, rahisi na anayewezekana, alikwenda na ukarimu wa moyo wake safi, lakini alipaswa kusubiri kwa muda mrefu. Hatimaye alizungumza na Askofu, lakini hakuaminika. Papa ameongeza kusema “Na mara nyingi sisi maaskofu…mara nyingi…Alikutana na Mama Yetu tena, ambaye alimfariji na kumwomba ajaribu tena.
Mhindi alirudi kwa Askofu na kwa shida sana kukutana naye, lakini kwa mara ya pili, baada ya kumsikiliza, alimfukuza na kutuma wanaume kumfuata. Hapa kuna juhudi, uthibitisho wa tangazo: licha ya bidii, zisizotarajiwa hufika, wakati mwingine kutoka kwa Kanisa lenyewe. Kiukweli, kutangaza haitoshi kushuhudia mema, bali ni muhimu kujua jinsi ya kubeba uovu. Tusisahau hili: ni muhimu sana kujua kwamba kutangaza Injili haitoshi kushuhudia mema, lakini ni muhimu kuweza kubeba maovu. Mkristo hutenda mema, lakini huvumilia mabaya. Yote mawili yanakwenda pamoja, hayo ndiyo maisha. Hata leo, katika maeneo mengi, ili kukuza Injili na kueneza tamaduni za injili, uvumilivu na subira zinahitajika, ni muhimu kutoogopa migogoro, sio kukata tamaa.
Baba Mtakatifu Francisko katika muktadha huo amefikiria nchi ambayo Wakristo wanateswa kwa sababu wao ni Wakristo na hawawezi kufuata dini zao vizuri na kwa amani. Juan Diego, akiwa amevunjika moyo, kwa sababu askofu alikuwa akimuahirisha, alimwomba Mama Yetu amwachilie na ateue mtu anayeheshimiwa na mwenye uwezo kuliko yeye, lakini alialikwa kuvumilia. Daima kuna hatari ya kupata mavuno fulani katika tangazo: kuna kitu kibaya na mtu anarudi nyuma, akivunjika moyo na labda kukimbilia katika uhakika wake mwenyewe, kama vile vikundi vidogo na katika ibada fulani za karibu. Kwa upande mwingine, Mama yetu, huku akitufariji, hutufanya tuendelee na hivyo kutufanya tukue, kama mama mwema ambaye, akifuata nyayo za mwanawe, anamwingiza katika changamoto za ulimwengu.
Juan Diego, hivyo kwa kutiwa moyo, alirudi kwa Askofu ambaye alimwomba ishara. Mama yetu alimuahidi, na kumfariji kwa maneno haya: “Usisumbue uso wako, usisumbue moyo wako: [...] “Je, mimi siko hapa, mama yako ni nani?" (ibid., 118-119). Papa ameongeza Hii ni nzuri, Mama yetu, mara nyingi tunapokuwa katika ukiwa, katika huzuni, katika shida, yeye pia anatuambia, moyoni mwake: "Si nipo hapa, mama yako ni nani?" Daima yuko karibu kutufariji na kutupatia nguvu ya kuendelea." Kisha alimwomba aende kwenye kilele kilicho kavu cha kilima ili kuchuma maua. Ilikuwa ni majira ya baridi, lakini licha ya hayo, Juan Diego alipata maua mazuri na kuyaweka katika vazi lake na kumpatia Mama wa Mungu, ambaye alimwalika kuyapeleka kwa Askofu kama ushahidi. Alikwenda, akingoja zamu yake kwa subira na mwishowe, mbele ya Askofu, alifungua tilma yake, ambayo watu wa asilia walikuwa wakijifunika nayo, alipofungua tilma yake iliyokuwa na maua tazama: picha ilionekana kwenye kitambaa, vazi la Mama, yule wa ajabu na aliye hai tunayemjua, ambaye machoni pake wahusika wakuu wa wakati huo bado wametiwa chapa.
Papa Francisko ameongeza kusema “Hapa kuna mshangao wa Mungu: wakati kuna kupatikana na, wakati kuna utii, anaweza kufanya jambo lisilotarajiwa, kwa nyakati na kwa njia ambazo hatuwezi kutabiri. Na kwa hivyo madhabahu iliyoombwa na Bikira ilijengwa na inaweza kutembelewa leo hii”. Juan Diego aliacha kila kitu na, kwa ruhusa ya Askofu, aliweka maisha yake wakfu katika madhabahu. Alikaribisha mahujaji na kuwainjilisha. Hiki ndicho kinachotokea katika madhabahu ya Maria, sehemu za kuhiji na mahali pa kutangaza, ambapo kila mtu anajisikia yuko nyumbani kwa sababu ni nyumba ya mama, na anahisi kutamani nyumbani, yaani, kutamani nyumbani ambako Mama wa Mbingu yupo.
Kwa hiyo huko imani inakaribishwa kwa njia rahisi, imani inakaribishwa kwa njia ya kweli, kwa njia inayopendwa na wengi, na Mama Yetu, kama alivyomwambia Juan Diego, anasikia machozi yetu na kuponya mateso yetu (taz. ibid., 32). Papa amesisitiza kuwa,“Tujifunze hivi: kunapokuwa na ugumu wa maisha, tunakwenda kwa Mama; na wakati maisha yana furaha, tunakwenda kwa Mama pia hii ni kuhiriki. Tunapaswa kwenda kwenye maeneo haya ya faraja na huruma, ambapo imani inaoneshwa katika lugha mama; ambapo ugumu wa maisha huwekwa mikononi mwa Mama na mtu anarudi kwenye maisha na amani moyoni, labda kwa amani ya watoto.