Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Sinfonische Dichtung
Ratiba Podcast
Vyombo vya ulinzi na usalama nchini Australia vimefanikiwa kumpiga risasi na kumuua Bwana Joel Cauchi mwenye umri wa miaka 40 kutoka Queensland kwa kusababisha mauaji ya watu sita. Vyombo vya ulinzi na usalama nchini Australia vimefanikiwa kumpiga risasi na kumuua Bwana Joel Cauchi mwenye umri wa miaka 40 kutoka Queensland kwa kusababisha mauaji ya watu sita.  (AFP or licensors)

Papa Francisko Asikitishwa na Mauaji Nchini Australia

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe ulioandikwa kwa niaba yake na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican kwenda kwa Askofu mkuu Anthony Fisher, anaeleza kusikitishwa kwake na mauaji haya na kwamba, anapenda kuonesha uwepo wake wakaribu kwa sala na sadaka yake. Baba Mtakatifu anapenda kuwafariji wale wote waliowapoteza ndugu, jamaa na wapendwa wao katika shambulio hili; marehemu wapate pumziko la milele na majeruhi wapone!

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S., Vatican.

Vyombo vya ulinzi na usalama nchini Australia vimefanikiwa kumpiga risasi na kumuua Bwana Joel Cauchi mwenye umri wa miaka 40 kutoka Queensland kwa kusababisha mauaji ya watu sita na wengine kumi na wawili kujeruhiwa vibaya, Jumamosi tarehe 13 Aprili 2024 huko Westfield Bondi Junction, kwenye duka kubwa mjini Sydney, nchini Australia. Inasemekana kwamba, Bwana Joel Cauchi alikuwa anakabiliana na changamoto ya afya ya akili na kwamba, shambulizi hili halina uhusiano wowote na vitendo vya kigaidi.

Watu sita wameuwawa na wengine 12 kujeruhiwa nchini Australia
Watu sita wameuwawa na wengine 12 kujeruhiwa nchini Australia   (AFP or licensors)

Ni katika muktadha huu, Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe ulioandikwa kwa niaba yake na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican kwenda kwa Askofu mkuu Anthony Fisher, anaeleza kusikitishwa kwake na mauaji haya na kwamba, anapenda kuonesha uwepo wake wakaribu kwa sala na sadaka yake. Baba Mtakatifu anapenda kuwafariji wale wote waliowapoteza ndugu, jamaa na wapendwa wao katika shambulio hili; anawaombea marehemu wapate pumziko la milele na majeruhi waweze kupata matibabu na hatimaye kurejea tena kuendelea na shughuli zao za kila siku. Mwishoni, Baba Mtakatifu Francisko anaiombea baraka, neema na faraja nchi ya Australia.

Maafa Australia
14 Aprili 2024, 13:52
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031