Tafuta

2024.09.08 Papa alikutana na Waamini ba wamisionari wa Vanimo nchini Papua New Guinea. 2024.09.08 Papa alikutana na Waamini ba wamisionari wa Vanimo nchini Papua New Guinea.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto) Tahariri

Ukristo, historia ya nyuso

Akiwa Papua New Guinea,Papa Francisko alikwenda Vanimo na kutimiza ndoto yake ya kukumbatia eneo la mbali zaidi ulimwenguni.

ANDREA TORNIELLI

Ukristo sio falsafa, wazo, mwongozo wa kanuni za maadili. Ukristo ni tukio lililounganishwa  na mshangao  na nyuso. Huko Vanimo na kisha katika kijiji cha mbali cha Baro, Dominika  alasiri moja yenye joto sana, tulipata uthibitisho wa hili kwa mara nyingine tena. Kulikuwa na mshangao na shukrani katika nyuso za Miguel De la Calle, Martín Prado na Tomás Ravaioli, wamisionari kutoka Argentina wa Shirika la  Neno lililofanyika mwili ambao wanatumia maisha yao kwa furaha kutangaza Injili kwenye viunga vya dunia, katika nchi hii ya ajabu ambayo ina rangi za michoro ya Paul Gauguin.

wakati wa kutumbuiza kikundi cha watoto
wakati wa kutumbuiza kikundi cha watoto

Kulikuwa na mshangao na shukrani katika uso wa Papa  Francisko, ambaye kwa karibu ya umri wa miaka 88, amefungwa kwenye kiti cha magurudumu, alipanda Hercules C130 ya Jeshi la Anga la Australia lililojaa vifurushi vya misaada na zawadi, ili kutimiza ndoto ya muda mrefu ya miaka kumi: ile ya kuwa hapa, pamoja nao na ya kukumbatia kwa macho na mikono ya baba mzee Mjesuit ambaye alikuja kuwa mchungaji wa ulimwengu wote wale wanaume wenye furaha, waliovalia mavazi meupe kama yeye, na juu ya watu wao wote. Wale watu waliojifunza kumjua Mama wa Yesu kutoka katika uso wa “Mama Luján” yaani, Mama Mtakatifu mlinzi wa Argentina.

Bikira maria wa Lujan
Bikira maria wa Lujan

Ilikuwa ni lazima kumwona Papa Francisko, akiwa ameketi katika chumba kidogo cha nyumba ya mbao iliyofunikwa na vyandarua wanakoishi wamisionari, huku akinywa mate akiwa ameketi karibu nao, baada ya umati wa wanaume, wanawake na watoto waliovaa nguo za rangi nyingi zilizofunikwa na manyoya machache au majani, na miili yenye kupakwa rangi. Kwa miaka mingi, Mrithi wa Petro amekuwa akiwasiliana na watu wa nchi yake ambao wanashuhudia upendo usio na masharti wa Mungu wa Yesu Kristo kati ya watu hawa. Hasa na mmoja wa hawa, Padre Martín, mmisionari huyo kijana, jana  hakuwa na neno la kumshukuru rafiki yake ambaye alipinga kila kitu na kila mtu kuweza kuwa hata kwa masaa machache tu na kuona kwa macho yake tamasha la Kanisa lililochanga na changamoto zake elfu zilizopatikana kwa furaha.

Kikundi cha wamisionari wa Vanimo
Kikundi cha wamisionari wa Vanimo

Hakuna uhaba wa matatizo huko Vanimo na Baro. Watu wanaishi katika mazingira hatarishi, bila maji ya bomba au umeme, na kuna dawa chache. Vurugu, ukabila na unyonyaji wa utajiri mkubwa wa madini na mbao unaofanywa na mashirika ya kimataifa ni ukweli. Mapadre wa Neno lililofanyika Mwili, kwenye ufuko huu wa Bahari ya Pasifiki ulio katikati ya msitu na miamba ya matumbawe, mnamo 2018 waliunda Bendi iliyoundwa na watoto na vijana. Miongoni mwa tani za vifurushi vilivyosafirishwa na Papa kwenye ndege ya kijeshi pia kulikuwa na ala  za muziki (violin na cellos.)

Papa alipokutana na waamini wa Vanimo

Papa Francisko, akiwa na furaha kama mtoto, aliweza kusikiliza nyimbo kadhaa. Wakati wa kuona tukio hilo mtu hawezi kujizuia kufikiria muujiza wa vile vijiji vya asili vya Paraguay vilivyoandaliwa na Wajesuit, pamoja na shule zao za uimbaji, ule mwangwi wake ambao unabaki katika vitabu vya historia na katika matukio kutoka katika filamu ya “Mission.” Chipukizi ndogo za Injili ambazo huchipuka polepole kati ya tamaduni za mababu na kurudia huruma, ukaribu, upole, upendo usio na masharti kuelekea mwisho wa walio sahaulika.

Papa alikutana na kikundi cha wamisionari
Papa alikutana na kikundi cha wamisionari

Maisha yanayotolewa kwa upendo hadi tone la mwisho. Furaha katika nyuso za wazee na watoto wengi wanaotabasamu. Furaha katika nyuso zilizochafuliwa na jua na jasho la wamisionari ambao leo hii wamevaa mavazi meupe kumkaribisha Askofu wa Roma, rafiki yao. Furaha katika uso wa Papa  Francisko, ambaye alipanda katika Ndege ya kijeshi ya C130, lakini ambapo angependa kubaki hapa.

Papa huko Vanimo kwa mujibu wa Dk Tornielli
09 September 2024, 15:13