Tafuta

Karibu watoto 17 wa Shule ya Msingi ya Bweni wameteteketa huko Nyeri nchini Kenya. Karibu watoto 17 wa Shule ya Msingi ya Bweni wameteteketa huko Nyeri nchini Kenya.  (ANSA)

Masikitiko ya Papa kwa watoto zaidi ya 17 waliuawa na moto huko Kenya

Baba Mtakatifu Francisko katika telegramu iliyotiwa saini na Kardinali Pietro Parolin,Katibu wa Vatican,anaelezea masikitiko yake kwa sababu ya moto uliozuka nchini Kenya na kusababisha wahanga,majeruhi na karibu watoto 70 waliopotea.Rais wa Nchi ametangaza maombolezo ya kitaifa ya siku tatu.

Vatican News

Masikitiko makubwa yalioneshwa na Baba Mtakatifu Francisko katika barua iliyotiwa saini na Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin iliyotumwa kwa Askofu Mkuu Antonio Muheria wa Nyeri, nchini Kenya, kwa sababu ya moto ambao watoto zaidi ya 17 wamepoteza maisha katika Shule ya Bweni ya Hillside Endarasha na karibu wengine 70 hawakupatikani wakiwemo wafanyakazi.

Ukaribu wa kiroho wa Papa

Baba Mtakatifu Francisko katika salamu zake ameonesha ukaribu wake wa kiroho kwa "wale wote wanaoteseka na athari za mkasa huo, hasa kwa majeruhi na familia zinazoomboleza.” Kwa hiyo, Papa “anazikabidhi roho za marehemu katika huruma ya upendo ya Mwenyezi Mungu” akitoa "sala zake kwa wale wote wanaojishughulisha na kutoa msaada na kuomba baraka za Bwana ili awape nguvu, amani na faraja."

Siku tatu za maombolezo

Moto huo katika Shule ya Msingi ya Bweni ya Hillside Endarasha ulizuka muda wa saa sita usiku, siku ya Alhamisi 5 Septemba 2024 kwenye shule hiyo ya bweni ambapo zaidi ya watoto 150 walikuwa wamelala. Shule hiyo, ambayo inakaribisha wanafunzi 800 wenye umri kati ya miaka 9 na 12 au 13, iko katika eneo la nusu vijijini,  takriban kilomita 170 kaskazini mwa mji mkuu Nairobi, Kenya. Kwa mujibu wa Mamlaka, watu 14 walijeruhiwa, huku watoto 70 wakiwa bado hawajapatikana, ingawa hii haimaanishi kuwa wamekufa au kujeruhiwa. Rais William Ruto hata hivyo alitangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kuanzia Jumatatu kwa kile alichokiita “msiba usiofikirika.”

Papa atuma salamu za rambi rambi Kenya
07 September 2024, 17:58