Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Rondeau (Andante grazioso)
Ratiba Podcast
2025.03.23  Salamu na baraka za Papa Francisko akiwa katika dirisha la Hospitalini Gemelli. 2025.03.23 Salamu na baraka za Papa Francisko akiwa katika dirisha la Hospitalini Gemelli.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto) Tahariri

Karibu nyumbani Papa!

Dk.Andrea Tornielli,Mhariri wetu Mkuu wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano anaandika tahariri yake kuhusu kurudi nyumbani kwa Papa:“Baada ya siku 38 Papa Francisko ameacha Hopsitali ya Gemelli.”

Andrea Tornielli

Zimepita siku 38 tangu tarehe 14 Februari, wakati papa Francisko alikuwa ameacha Vatican kwa ajili ya kulazwa katika Hospitali ya Gemelli. Majuma magumu kwa mgonjwa wa miaka 88 aliyekuwa ameshikwa na ugonjwa wa Mkamba wa pande mbili. Tahari za madaktari hazikunyamaza kuelezea hali ngumu, mgogoro ambao alipitia, mgumu sana katika mtazamo wa vipimo vya kliniki. Lakini siku alizopitia zilikuwa hasa za kusindikizwa na mto wa sala kwa ajili ya afya: sala binafsi, sala za kijumuiya, rozari, oya misa. Waliosali kwa ajili ya Papa hawakuwa wakatoliki tu, na wala wakristo tu. Walisali kwa ajili ya Papa hata wanawake na wanaume wa dini nyingine. Walituma mawazo mazuri na matashi mema hata watu wasio amini. Ni kwa ajili ya watu wote katika sala ambao kwa salamu fupi leo hii imependwa na imefikiriwa.

Tumeishi na Askofu wa Roma kwa siku hizi ndefu za mateso, tulisubiri, tulisali, tulishikwa hisia kali wakati rehe 7 Machi, Papa Francisko alipopenda sauti yake iweze kuwafikia wote, kwa kuwashukuru waamini waliokuwa katika sala kwenye Uwanja wa Mtakatifu Petro, na waliokuwa wameunganishwa nao ulimwenguni kote. Tulitiwa moyo, usiku wa Dominika ya tarehe 16 Machi, wakati kwa mara ya kwanza tulioona hata kama ni upande wa mgongo wake, picha ambayo alikuwa akisali mara baada ya maadhimisho ya misa katika kikanisa kilichopo Ghorofa ya 10 ya Hospitali ya Gemelli. Baada ya kuhangaika sana lakini pia uaminifu mwingi na kujikabidhi kwa mpango wa Yule anayetupa sisi maisha kila dakika na ambaye kila dakika anaweza kutuita kwake, leo hii tumemuona. Tumepokea kwa upya baraka yake katika siku ambayo amerudi tena mjini Vatican.

Kutoka katika chumba cha hospitali kwa majuma haya, Papa Francisko alitukumbusha kuwa maisha ni ya hadhi yanayotakiwa kuishi kila dakikira na kila dakika yanaweza kuombwa. Alitukumbusha kuwa mateso na udhaifu unaweza kugeuka kuwa fursa ya kushuhudia kiinjili, kwa ajili ya kutangaza Mungu ambaye anakuwa Mwanadamu, na anateseka na sisi kwa kukubali kuwambwa juu ya Msalaba. Tunamshukuru kwa ajili ya kusema akiwa katika chumba cha hospitali, kuwa vita vilionekana bado kuwa vya kipuuzi, kwa ajili ya kutueleza kwamba ni lazima tuipokonye dunia silaha na kwa hiyo tusiiweke tena katika kujaza ghala zake za silaha na vyombo vipya vya kifo; kwa ajili ya kusali na kuteseka kwa matueso yake kwa ajili ya amani kiasi cha kuwa hatarini leo. Karibu nyumbani Baba Mtakatifu!

Tahariri ya Dk Tornielli: Karibu Papa nyumbani
23 Machi 2025, 12:27
Prev
March 2025
SuMoTuWeThFrSa
      1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031     
Next
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930