Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
L'Ange aux parfums
Ratiba Podcast
Papa Francisko anaendelea  na matibabu hospitalini Gemelli,Roma. Papa Francisko anaendelea na matibabu hospitalini Gemelli,Roma.  (ANSA)

Nia ya Papa ni kuchungulia dirishani Dominika 23 Machi baada ya saa 6 kwa ajili ya baraka!

"Papa anapanga kuonekana Dominika tarehe 23 Machi 2025 baada ya saa 6.00 kamili,masaa ya Ulaya na (baada ya saa 8 kamili masaa ya Afrika Mashariki na Kati)kwa ajili ya kutoa baraka."Hivyo ndivyo Ofisi ya Habari Vatican,Jumamosi tarehe 22 Machi 2025 ilivyoripoti.Hali ya afya ya Papa ni shwari,anaendelea na matibabu yake na anajitolea kufanya kazi ndogo na maombi.

Vatican News

Papa Francisko anatarajia kuchungulia kutokea  katika dirisha la Hospitali ya Gemelli kesho tarehe 23 Machi 2025, muda mfupi baada ya saa 6:00 kamili mchana saa za Ulaya (baadaye kidogo ya saa 8 kamili mchana saa za Afrika Mashariki na Kati), ili kusalimia na kutoa baraka zake. Nakala ya tafakari ya Malaika wa Bwana itatolewa kama katika Dominika zilizopita. Vyombo vya habari vya Vatican vitakuwepo kwa ajili ya huchukuaji na usambazaji wa picha hizo. Taarifa ya Ofisi ya Vyombo vya habari, Vatican imeripotii leo hii, Jumamosi tarehe 22 Machi 2025.

Taarifa za afya Papa, Mchi 21

Jana, Ijumaa jioni tarehe  21 Machi 2025,  Ofisi ya vyombo vya habari, Vatican  ilitoa sasisho kuhusu hali ya afya ya Papa  Francisko, ambayo bado ni thabiti na uboreshaji mdogo katika mifumo yake ya mazozi ya viungo  na kupumua. Siku za Papa zilipita kati ya tiba ya madawa na tiba ya mazozi ya viungo na  ya kupumua pamoja na maombi na kazi kidogo.

Papa Francisko hakupokea wageni wowote. Wakati wa usiku hatumii tena uingizaji hewa ya mitambo na barakoa, bali oksijeni ya mtiririko wa juu  kwa kutumia pua na wakati wa mchana hatumii mtiririko wa juu sana bali kidogo.


Taarifa inayofuata ya matibabu inatarajiwa si zaidi ya Jumatatu. Wakati huo huo, tunapoendelea kumwombea afya njema jioni ya Jumamosi tarehe 22 Machi 2025, mida ya saa 1.30, kama kawaida ya siku hizi, sala ya  Rozari Takatifu  itaongozwa na Monsinyo Giordano Piccinotti, rais wa Utawala wa Urithi wa Makao ya Kitume, Vatican.

22 Machi 2025, 12:20
Prev
March 2025
SuMoTuWeThFrSa
      1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031     
Next
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930