Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Allegro con spirito
Ratiba Podcast
Ulinzi wa kila mtoto alie hatarini Ulinzi wa kila mtoto alie hatarini 

Papa:ikiwa mtoto au mtu aliye hatarini yuko salama,Kristo anahudumiwa na kuheshimiwa!

Katika ujumbe kwa washiriki wa Mkutano wa Mwaka wa Tume ya Kipapa kwa ajili ya Ulinzi wa Watoto,Papa Francisko anasisitiza juu ya kusaidia waathirika wa nyanyaso kwa makaribisho na kutunza majeraha ya kiroho.Anakumbusha kwamba"mazoezi ya kuzuia ni ahadi na dhamira ya mazingira salama kwa kila mtoto na kila mtu aliye katika mazingira magumu kwa sababu kuzuia unyanyasaji si blanketi la kuenea juu ya dharura,lakini moja ya misingi wa kujenga jumuiya aminifu kwa Injili."

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Baba Mtakatifu Francisko ametuma ujumbe wake kwa washiriki wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa Tume ya Kipapa ya Ulinzi wa Watoto ambao ulifunguliwa Jumatatu  tarehe Machi 24 na utahitimishwa Ujumaa tarehe 28 Machi 2025. Ujumbe huo uliotiwa saini huko Hospitalini Gemelli  tarehe 20 Machi 2025  Papa Francisko. Papa anawatumia salamu zake za uchangamfu na “maelekezo fulani kwa ajili ya huduma yao muhimu. Hakika ni kama “oksijeni” kwa Makanisa ya mahalia pamoja na jumuiya za kidini, kwa sababu popote mtoto au mtu aliye hatarini akiwa  salama, hapo mnamtumikia na kumheshimu Kristo.” Katika utaratibu wa kila siku wa kazi yenu- hasa katika maeneo yaliyokosa fursa zaidi - ukweli wa kinabii unakuwa ukweli hasa kuzuia unyanyasaji si blanketi la kutandazwa juu ya dharura, lakini ambayo ni moja ya misingi ambayo juu yake inaweza kujenga jumuiya aminifu kwa Injili. Kwa hili, ninatoa shukrani zangu."

Sera za kuzuia katika jumuiya mbali mbali

Papa Francisko anaeleza umuhimu wa  jitihada zao zinavyopaswa kuwa: “ Kazi yenu haiwezi kupunguzwa kuwa itifaki za kutumiwa, lakini inayokuza ulinzi: muundo unaoelimisha, kuangalia kuzuia, kusikiliza na ambayo inarejesha  heshima.” Aidha Papa alisema kuwa wao wanapoanzisha sera za kuzuia, hata katika jumuiya za mbali zaidi, waaandika ahadi: kwamba "kila mtoto, kila mtu aliye hatarini, atapata mazingira salama katika jumuiya ya kikanisa. Hii ndio injini ya kile kinachopaswa kuwa kwetu ubadilishaji muhimu.”

Maombi matatu ya Papa:ushirikiano na Curia Romana,ukarimu na kujenga ushirikiano na vyombo vya nje

Papa Francisko katika Ujumbe wake anatoa  ombi lake kuwa: “Leo, ninawaomba ahadi  ya mambo matatu: 1. Kuendeleza kazi ya pamoja na  Mabaraza ya Curia Romana;  2. Kutoa ukarimu na kutunza majeraha ya roho kwa wahanga na walionusurika, kwa mtindo wa Msamaria mwema. Kusikiliza kwa sikio la moyo, ili kwamba kila ushuhuda haupati rejista ya kukusanywa, lakini  huruma ya kina ambayo  kwayo kuna kuzaliwa upya;  3. Kujenga ushirikiano na vyombo vilivyo nje ya Kanisa - mamlaka za kiraia, wataalamu, vyama - ili ulinzi uweze kuwa lugha ya ulimwengu wote.

Kwa miaka 10 wamewezesha mtandao kukua ndani ya Kanisa

Kwa kuhitimisha ujumbe huo Baba Mtakatifu anabainisha kwamba:“ Katika miaka hii kumi, mmewezesha mtandao wa usalama kukua ndani ya Kanisa. Muendelee! Mundelee kuwa walinzi wanaokesha ulimwengu unapolala. Roho Mtakatifu, mwalimu wa kumbukumbu hai, atulinde na majaribu ya kuondoa huzuni badala ya kuyaponya. Asante kwa ukumbusho wenu katika maombi. Mimi pia ninawasindikiza na ninamwomba Bwana na Bikira Mwenyeheri  awasimamie, ili muendelee na safari yenu kwa ari na matumaini," anahitimisha Papa.

Ujumbe wa Papa kwa Tume ya Ulinzi wa Watoto

 

25 Machi 2025, 10:49
Prev
March 2025
SuMoTuWeThFrSa
      1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031     
Next
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930