Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Rondo (Vivace)
Ratiba Podcast
2025.03.22 Kardinali Battaglia akisoma Ujumbe wa Papa wakati wa Misa ya Hija ya Kijubilei kwa jimbo la Napoli na majimbo mengine. 2025.03.22 Kardinali Battaglia akisoma Ujumbe wa Papa wakati wa Misa ya Hija ya Kijubilei kwa jimbo la Napoli na majimbo mengine.   (Vatican Media)

Papa:kukusanyika kwenu ni kukumbatia mwaliko wa Yesu wa kuingia mlango mwembamba!

Papa Francisko alituma ujumbe kwa washiriki wa hija ya Jubilei ya Jimbo kuu la Napoli nchini Italia na majimbo mengine akiwahimiza kuwa “Kuvuka Mlango Mtakatifu ili Kuanzisha Upya Umoja katika Upendo.Maandiko hayo yalisomwa na Kardinali Domenico Battaglia,Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la mji wa Napoli,wakati wa adhimisho la Ibada ya Misa Takatifu mbele ya Kanisa kuu la Mtakatifu Petro,Jumamosi tarehe 22 Machi 2025.

Na Angella Rwezaula – Vatican

Ni kutoka katika Hospitali ya Gemelli, jijini  Roma ambapo Baba Mtakatifu Francisko alitia saini ujumbe wake wa ukaribu kwa mahujaji walioshiriki katika hija ya Jubilei ya Jimbo kuu la Napoli lakini ambayo pia imewahusu waamini wengi, wengi wao wakitoka katika majimbo mengine ya Italia, ambapo siku ya Jumamosi tarehe 22 Machi 2025 walivuka Mlango Mtakatifu wa kanisa Kuu la Mtakatifu Petro. Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe huo aliwaelekea kaka na dada wote wa Napoli na majimbo mengine. Aliwasalimu maaskofu wao katika fursa hiyo ya Hija ya kijubilei kijimbo ambayo wamehitimiza.

Kardinali Battaglia akisoma ujumbe wa Papa

Kardinali Battaglia akisoma ujumbe wa Papa(Vatican Media)

Kukumbatia mwaliko wa Yesu wa kuingia mlanngo mwembamba

Papa alibainisha kuwa katika Jubilei hiyo “inaonesha umoja unaowakusanya ninyi kama jumuiya inayowazunguka Wachungaji wenu na Askofu wa Roma, pamoja na kujitolea kukumbatia mwaliko wa Yesu wa kuingia “kupitia mlango ulio mwembamba”(Mt 7:13). Upendo uko hivi: unatuunganisha na kutufanya kukua pamoja. Kwa sababu hii, ingawa tumepitia njia mbalimbali, imewaleta ninyi hapo pamoja kwenye kaburi la Petro, ambapo mnaweza kutoka tena na nguvu zaidi katika imani na umoja zaidi katika upendo.”

Misa ya wanahija wa kijubilei kutoka Napoli na majimbo mengine mengi

Misa ya wanahija wa kijubilei kutoka Napoli na majimbo mengine mengi(VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Papa ameshukuru sala anazoombewa

Papa Francisko katika ujumbe huo aidha alibainisha kuwa: “Katika siku hizi nimeona kuungwa mkono na ukaribu wenu hasa kwa maombi mliyonisindikiza. Kwa hiyo, hata kama siwezi kuwa pamoja nanyi kimwili, ninawaonesha furaha yangu kuu kwa kujua kwamba mmeunganishwa pamoja nami na ninyi wenyewe katika Bwana Yesu kama Kanisa.” Papa alihitimisha kwa kuwabariki kuwa “Ninawabariki na kuwaombea. Na ninapendekeza kwenu: ninyi  pia muendelee kuniombea. Asante.”

Misa ya wanahija kutoka Napoli na majimbo mengine

Misa ya wanahija kutoka Napoli na majimbo mengine (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Ujumbe wa Papa kwa wanahija wa Napoli

 

22 Machi 2025, 14:43
Prev
March 2025
SuMoTuWeThFrSa
      1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031     
Next
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930