Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Havanaise
Ratiba Podcast
2025.03.23 Salamu ya Papa na baraka katika dirisha la Hospitali ya Gemelli,Roma. 2025.03.23 Salamu ya Papa na baraka katika dirisha la Hospitali ya Gemelli,Roma.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Ulimwengu unamwona Papa tena,salamu kutoka Gemelli: “Asanteni nyote"

Papa Francisko amechungulia kwa mara ya kwanza tangu kulazwa kwake hospitalini kabla ya kuiacha alipolazwa tangu Februari 14.Salamu,baraka kwa mikono yake juu ya watu 3000 waliokusanyika katika uwanja huku wakipiga makofi na kutaja jina lake.Baba Mtakatifu alimsalimia mwanamke Carmela,mwenye umri wa miaka 78 aliyekuwa ameshikilia maua ya njano na kumsifu.Mwandishi wetu wa Vatican News amekuwa na mengi ya kueleza.

Na Salvatore Cernuzio – Roma

 

“Asante ninyi nyote”

 

Huyo hapa Papa, hapa anatokea tena kwa waamini 3,000 waliokusanyika tangu asubuhi katika uwanja wa Hospitali ya Gemelli ambao katika siku hizi 38 za kulazwa hospitalini kumeonekana mlolongo usiokatizwa wa maombi kwa ajili ya  kupona kwake. Yalikuwa ni maneno machache kutoka kwenye balcony ya ghorofa ya tano, akionesha uso uliochoka, mikono juu ya magoti na iliyoinuliwa kupungia na  kubariki. Kidokezo cha tabasamu katika kuona na kusikia umati huo ukipiga kelele: "Francesco, Francesco!", "Tunakupenda!", "Tuko hapa kwa ajili yako!"

Papa akiwa katika dirisha la Hospitali Gemelli
Papa akiwa katika dirisha la Hospitali Gemelli   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Salamu kwa Carmela, "mwanamke mwenye maua ya manjano" "Asante nyote!" Papa alisema kwa sauti dhaifu. Salamu ilitarajiwa, lakini Papa alitaka kuonekana na kusikilizwa. Macho yake yalitazama  upande mmoja wa uwanja hadi mwingine, basi, kama ilivyo kawaida yake, na alizingatia jambo moja: Bi Carmela Mancuso, mwenye umri wa miaka 78 kutoka Calabria, aliyekuwa  mstari wa mbele akielekeza kwenye balcony ndogo, akiwa ameshikilia shada la maua ya njano. Aliondoka katika kituo cha Mtakatifu Pietro kwenda Gemelli. Na amefanya hivyo karibu kila siku kwa zaidi ya mwezi mmoja, lakini pia amefanya mara nyingi wakati wa Katekesi  kila  Jumatano. "Na ninamwona mwanamke huyo mwenye maua ya manjano! Ni mwema!" Papa alisema.

Katika Uwanja wa Mtakatifu Petro waamini walifuatilia yaliyokuwa yakiendelea  Gemelli
Katika Uwanja wa Mtakatifu Petro waamini walifuatilia yaliyokuwa yakiendelea Gemelli   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Mzunguko wa makofi, kwaya ya "Uishi muda mrefu Papa”, ilisikika. Bi Carmela yule yule aliyeinamisha kichwa chake, akaburuzwa chini na uzito wa machozi yake. "Sijui la kusema. Asante, asante, asante, kwa Bwana na Baba Mtakatifu. Sikufikiri kuwa 'nimeonekana' hivyo," alitoa maoni yake mara moja baadaye kwa vyombo vya habari vya Vatican. "Alitakiwa kutoa baraka na badala yake aliona shada langu la waridi. Namtakia apone haraka na arudi kwetu kama hapo awali."

Shada la Maua ya Bi Carmela
Shada la Maua ya Bi Carmela   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Kukumbatia watu

Kulikua na matashi mema yaliyotolewa na wauguzi, madaktari, na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kikatoliki waliokusanyika ndani. Kulikuwa na  waamini wa mataifa mbalimbali, Shirika la Auxilium ambao waliinua kabla ya saa 6 kamili bango kubwa na bendera kutoka duniani kote na wito wa amani. Kulikuwa na mtu aliyefikisha miaka 75 jana ameshikilia ishara ambayo alimkabidhi Papa  Francisko kwa maombezi ya mtangulizi wake Yohane  Paulo II. Na kulikuwa na  kikundi ambacho kutoka Uwanja wa Mtakatifu Petro kilichukua msalaba wa Jubilei - ule uliotumiwa kwa hija kwenye Mlango Mtakatifu - na kufika hadi Gemelli: "Ni muhimu kuwa hapa,” walibainisha. Kulikuwa na  Emanuela na Adam, pamoja na watoto wao watatu, ambao baada ya Misa “karibu” walitaka kuwachukua watoto kumsalimia Papa Francisko: “Tulisali kila siku mezani kwa ajili yake, ilikuwa sawa kwamba walimwona,” baba huyo alisema. Kisha kulikuwa na Sr Geneviéve Jeanningros, mtawa wa Bustani ya Luna huko Ostia, anayejikitia na shughuli za  uchungaji  Roma na kikundi cha Sinti lakini pia cha mashoga na watu waliobadili jinsia. Jamaa wa zamani wa Papa ("mtoto wa kutisha", anamwita) ambaye huenda kumsalimia kila Jumatano kwenye katekesi katika uwanja wa Mtakatifu Petro au katika Ukumbi wa Paulo VI. “Nisingeweza kungoja kwamba Papa Francisko ajitokeze na kutoka," alitoa maoni kwa vyombo vya habari vya Vatican. "Hatukuweza kuvumilia tena. Tunamtakia kila la heri. Heri njema.”

Kuaga wakati wa kutoka hospitalini kupitia Mtakatifu Maria Mkuu

Mara tu baada ya kutoka kwenye balcony, umati wa watu ulisogea kuelekea lango la Gemelli ili kumnasa Papa atoke akiwa katika mtindo wake wa kawaida na ambao sasa unajulikana sana, wa Gari la Fiat 500L nyeupe. Salamu na nyimbo zaidi ziliambatana na njia ya Papa ndani ya gari, na madirisha yakiwa yamefungwa. Mwelekeo ni Mtakatifu Maria Mkuu  katika basilika  ambayo haijawahi hata mara moja - baada ya safari ya kimataifa au upasuaji na kulazwa hospitalini - Jorge Mario Bergoglio ameshindwa kutembelea kusali kwa Salus Populi Romani na kumshukuru kwa ulinzi wake.

Baada ya kutoka Hospitalini alielekea Kanisa Kuu la Mtakatifu Maria na baadaye nyumbani
Baada ya kutoka Hospitalini alielekea Kanisa Kuu la Mtakatifu Maria na baadaye nyumbani   (ANSA)

Kabla ya kutokea kwenye balcony ya hospitali, Papa Francisko alitaka kuwasalimu kwa ufupi wafanyakazi na wasimamizi wa Chuo Kikuu cha Kikatoliki na Gemelli Polyclinic: mkuu wa Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Moyo Mtakatifu, Profesa Elena Beccalli; rais wa Mfuko wa  Hospitali ya Chuo Kikuu cha Agostino Gemelli IRCCS, Dk. Daniele Franco; pia Mkuu wa Kitivo cha Tiba na Upasuaji cha Chuo Kikuu cha Kikatoliki, profesa Antonio Gasbarrini; makamu  rais wa Mfuko, Giuseppe Fioroni; mkurugenzi mkuu, Marco Elefanti, msaidizi mkuu wa kikanisa wa Chuo Kikuu, Askofu Claudio Giuliodori, na Profesa Sergio Alfieri, mkurugenzi wa Idara ya Sayansi ya Tiba-Upasuaji ya Policlinico na mkuu wa timu ya matibabu ya Gemelli; mkurugenzi wa afya wa Mfuko wa Hospitali ya  Gemelli, Andrea Cambieri.

Umati ukimshangilia Papa
Umati ukimshangilia Papa
Papa Francisko kuonekana kwenye dirisha la Hospitali baada ya siku 38
23 Machi 2025, 14:41
Prev
March 2025
SuMoTuWeThFrSa
      1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031     
Next
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930