Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Terramoto - Presto e con tutta la forza
Ratiba Podcast
2025.04.06 Papa Francisko awabariki waamini waliounganika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro katika fursa ya Jubilei ya Wagonjwa na Ulimwengu wa kiafya. 2025.04.06 Papa Francisko awabariki waamini waliounganika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro katika fursa ya Jubilei ya Wagonjwa na Ulimwengu wa kiafya.  (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Papa ashangaza wanajubilei kwa kufika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro na kushukuru!

Papa Francisko amewabariki na kuwashukuru waamini mwishoni mwa Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya Jubilei ya Wagonjwa na Ulimwengu wa Afya:"Asanteni sana!"Kabla ya kufika kwenye uwanja alifanya sakramenti ya kitubio katika Basilika ya Mtakatifu Petro na baadaye akapita mlango Mtakatifu,kwa mujibu wa taarifa za Ofisi ya Vyombo vya Habari Vatican.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Ulikuwa ni mshangao mzuri mwishoni mwa Misa ya Jubilei kwa wagonjwa na ulimwengu wa huduma za afya hasa wa kuwasili kwa Baba Mtakatifu Francisko kwenye uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, Dominika tarehe 6 Aprili 2025. Katika kiti cha magurudumu, akifuatana na muuguzi wake wa kibinafsi Massimiliano Strappetti. Ni yeye aliyemepeleka kwenye madhabahu, ambapo, baada ya baraka ya mwisho ya mshereheshaji, Askofu Mkuu Fisichella, alitangaza salamu fupi: Dominika  njema kwa kila mtu, asante sana!" Kwa hisia za wote waliokuwepo uwanjani, na wasomaji kisha wakasambaza ujumbe wake wa shukrani.

Papa akiwa mbele ya madhabahu
Papa akiwa mbele ya madhabahu   (Vatican Media)

Katika ujumbe huo Papa Francisko anawasalimu kwa upendo wote walioshiriki katika maadhimisho haya na kuwashukuru kwa dhati kwa sala iliyoinuliwa kwa Mwenyezi Mungu kwa ajili ya afya yake, akitumain kwamba hija ya Jubilei hiyo itakuwa na matunda tele". Kisha ametoa baraka za kitume, anazozipeleka “kwa wapendwa, wagonjwa na wanaoteseka, pamoja na waamini wote waliokusanyika leo”.  

Papa akipita mlango Mtakatifu
Papa akipita mlango Mtakatifu   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)

Kabla ya kutoka nje katika Uwanja, kwa mujibu wa Ofisi ya Habari ya Vatican iliripoti, kwamba Papa alipokea sakramenti ya upatanisho katika Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, na kukaa kitambo kwa sala na baadaye akavuka  Mlango Mtakatifu. Kwa hiyo Papa aliungana na wanahija wa Jubilei ya wagonjwa na wa Ulimwengu wa kiafya.

Askofu Mkuu Fisichella akimpa salamu
Askofu Mkuu Fisichella akimpa salamu   (VATICAN MEDIA Divisione Foto)
Papa aliungama

 

06 Aprili 2025, 15:24
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031