Tafuta

Majonzi makuu na uchungu huko Bucha nchini Ukrane kutokana na mauaji ya kinyama. Majonzi makuu na uchungu huko Bucha nchini Ukrane kutokana na mauaji ya kinyama. 

Kard Parolin:Ni muhimu kuzuia mwendelezo wa vita Ukraine

Katibu wa Vatican akiwa kando ya tukio katika Radio Vatican ametoa maoni yake juu ya habari za hivi karibuni kutoka nchi ya Ulaya Mashariki na kuthibitisha uwezekano wa safari ya Papa kwenda Kiev:”Sio marufuku,ikiwa tunafikiria kwamba inaweza kuchangia mwisho wa vita.Na kuhusu mkutano na Kirill ulio kwenye maadalizi:Amesema awanatafuta eneo lisilo na upande wowote.Na juu ya vifo huko Bucha amesema ni jambo lisiloelezeka.

Na Angella Rwezaula - Vatican

Kila kitu lazima kifanyike ili kuepusha kuongezeka kwa ghasia nchini Ukraine. Kardinali, Pietro Parolin, Katibu wa Vatican amerejea kuzindua ombi la amani katika nchi hiyo ya Ulaya Mashariki, bila kuondoa dhana ya safari ya Papa kwenda Kiev, ambayo  Papa Francisko mwenyewe alisema ilikuwa mezani. “Safari sio kizuizi, inaweza kufanywa. Ni suala la kuona ni matokeo gani safari hii inaweza kuwa nayo, kutathmini iwapo kweli inaweza kuchangia mwisho wa vita,” alisema Kardinali kwa waandishi wa habari aliyekutana naye nje ya Jumba la  Pio, ambayo ni makao makuu ya Radio Vatican, ambako alishiriki katika uwasilishaji wa mpango wa media kuhisiana na suala la uelewa wa Autism' au Usonji' Kardinali Parolin alihojiwa juu ya uthibitisho wa hivi karibuni wa  NATO ya kimataifa na katibu wake mkuu, Jens Stoltenberg , aliyesisitiza  juu ya kanuni ya ulinzi halali, lakini wakati huo huo akatoa wito  kwamba kila kitu kifanyike ili kuepuka kuongezeka kwa vita: Jibu la kisilaha kwa namna ambayo daima inaonesha uchokozi, kamaKatekisimu ya Kanisa Katoliki inavyotufundisha, inaweza kusababisha kupanuka kwa mzozo ambao unaweza kuwa na matokeo mabaya na ya kuua.  Matumaini yake ni kwamba kila mtu atarudi kwenye sababu na kutafuta njia ya mazungumzo ya kuhitimisha safari hii bila kurudi.

Picha za kutisha za maiti zilizotawanywa huko Bucha nchini Ukraine

Kardinali Parolin alitoa maoni yake kwa uchungu juu ya picha za ukatili zilizotokea huko Bucha, mji ulioko kilomita sitini kutoka Kiev, ambao umekuwa eneo la kile ambacho Papa amebainisha kuwa nimauaji,  huku miili ya raia ikiwa imetawanyika mitaani. “Haielezeki kuwa hii inaendelea dhidi ya raia. Ninaamini kweli, kama ilivyooneshwa na wengi, kwamba vipindi hivi vinaashiria mabadiliko katika vita hivi. Na ninatumaini kwamba wataiweka alama kwa maana chanya, ambayo ni wanafanya kila mtu atafakari juu ya hitaji la kukomesha mapigano haraka iwezekanavyo na sio kwamba wanafanya misimamo migumu kama wengine wanaogopa”.

Safari inayowezekana ya Papa kwenda Kiev

Katika hali hiyo hiyo, Katiby  alijibu swali kuhusu fursa ya Papa kwenda katika mji mkuu wa Ukraine. “Lazima kuwe na masharti. Ambayo yanaonekana kuwa pale, kwa sababu kwa upande wa Ukraine siku zote tumepewa uhakikisho wa kutosha kwamba hakutakuwa na hatari na kumbukumbu inafanywa kwa safari zinazofanywa na viongozi wengine na ambazo bado zinafanywa. Inaonekana kwangu kuwa rais wa Bunge la Ulaya amekwenda, rais wa Tume atakwenda”. Ninaamini kwamba mwishowe aafari ya kwenda Kiev sio kizuizi, inaweza kufanywa, Kardinali alisema. Walakini, matokeo yanatathminiwa. Na kati ya mahusiano haya na Kanisa la Kirthodhasingekwenda kwa ajili ya kuwa upande mmoja au mwingine  kama alivyokuwa akifanya katika hali hii ambayo imetokea. Walakini, kipengele hiki lazima pia kuzingatiwa katika kuzingatia kimataifauwezekano wa kufanya safari au la”.

Mkutano na Kirill

Bado katika muktadha wa uhusiano na Patriaki wa Moscow, katibu wa Vatican  i alithibitisha kwamba mipango fulani ilikuwa tayari imeanza kufanya mkutano kati ya Papa na Patriaki Kirill, baada ya ule wa tarehe 12  Februari 2016 huko Cuba. “ Ninachoelewa, maandalizi haya yanaendelea, alisema, akielezea kwamba utafiti kwa sasa uko kwenye msingi usio na upande wowote. “Hii ndiyo hali. Lakini hakuna kinachoamuliwa. Tunafanya kazi, kwa upande wetu, lakini zaidi ya yote na Baraza la Kipapa la Kuhamaisha Umoja wa Kikristo ambalo ni Baraza lenyewe lenye uwezo wa masuala hayo”.

Diplomasia Vatican haichoki kutafuta nchi za upatanisho

Akizungumzia kazi ya diplomasia ya Vaticani,  kazi isiyo na kikomo, kama ilivyosemwa na Papa Francisko kwenye safari ya ndege ya kurudi kutoka Malta Kardinali Parolin alielezea kwamba, ingawa hakuna mipango maalum  kwa sasa, uwezekano uliotolewa bado unaendelea, wakati fulani uliopita kwa shughuli ya upatanishi au aina nyingine yoyote ya uingiliaji kati ambayo inaweza, kwa upande mmoja, kuwezesha usitishaji mapigano na, kwa upande mwingine, kuanza kwa mazungumzo”. Kwa sasa  tunafikiria ikiwa kuna njia nyingine za kutafsiri uwezekano huu katika mipango thabiti zaidi, pia kwa sababu toleo hili lazima lipate uwezekano kwa pande zote mbili”. Dhana halisi pia inasalia kuwa safari ya kwenda Kiev na Askofu Mkuu  Paul Richard Gallagher, katibu wa Atican wa Mahusiano na  Ushirikiano na Mataifa. Akiwa amealikwa hata kabla ya kuzuka kwa vita, ndiyo maana alilazimika kughairi safari hiyo, Gallagher, alisema  Kardinali Paroli ataweza kuwa Ukrainekatika siku za usoni. Sidhani, hata hivyo, kwamba tarehe imepangwa”, Alihitimisha.

08 April 2022, 17:41