Tafuta

2022.12.03  Mti mrefu na Pango  vilivopambwa katika Uwanja wa Mtakatifu Petro, Vatican kwa ajili ya Siku Kuu ya Noeli 2022.12.03 Mti mrefu na Pango vilivopambwa katika Uwanja wa Mtakatifu Petro, Vatican kwa ajili ya Siku Kuu ya Noeli 

Uzinduzi wa Pango&mti wa Noeli uliopambwa katika uwanja wa Mt.Petro

Taa za Pango ambazo zilionesha vizuri sanamu kubwa zilizochongwa kwa mkono za mbao na kuwasha taa katika mti mrefu wa mapambo jioni tarehe 3 Desemba 2022 mjini Vatican,vilionesha tamasha zuri kwa washiriki katika Uwanja wa Mtakatifu Petro.Wakati huo afla ya uzinduzi ilifanyika katika Ukumbi wa Paulo VI kutokana hali mbaya ya hewa.

Na Angella Rwezaula; – Vatican.

Kutokana na hali mbaya ya hewa, sherehe za uzinduzi wa pango na  kuwashwa taa katika mti wa  mapambo ya Noeli vilivyopo kwenye viwanja vya Mtakatifu Petro mjini Vatican Jumamosi jioni tarehe 3 Desmba 2022 na ilifanyika katika ukumbi wa Paul VI. Kardinali Fernando Vérgez Alzaga, Rais wa serikali ya  mji wa  Vatican aliongoza hafla hiyo iliyohudhuriwa na Sista Raffaella Petrini, Katibu msaidizi wa Vatican, na wajumbe kutoka Sutrio na Rosello, maeneo hayo mawili, moja huko Friuli na  huko Abruzzo, ambapo Pango na Mti mzuri vilitokea. Hata hivyo Jumamosi asubuhi tarehe 3 Desemba ziliwasilishwa rasmi zawadi zao  kwa Papa Francisko wakati wa mkutano wao pia ambao  ilihudhuriwa na ujumbe wa serikali ya Guatemala ambao mwaka huu ulitoa zawadi ya Pango iliyopambwa katika Ukumbu wa Paulo VI. Ni uwakilishi wa Kuzaliwa kwa Kristo unaoundwa na  Familia Takatifu. Familia na malaika watatu waliotengenezwa na mafundi wanaoheshimu mila na utamaduni wa Guatemala, kwa vitambaa vikubwa vya rangi na sanamu za mbao.

Uzinduzi wa Pango na kuwasha mti wa mapambo ya siku kuu ya Noeli katika uwanja wa Mtakatifu Petro.
Pango na Mti wa mapambo ya Siku Kuu ya Noeli mjini Vatican
Pango na Mti wa mapambo ya Siku Kuu ya Noeli mjini Vatican

Sherehe hiyo ilifunguliwa kwa wimbo wa Taifa wa  Vatican ulioimbwa na Bendi ya Kikosi cha Ulinzi. Baadaye Kardinali Vérgez Alzaga alitoa salamu zake kwa kushukuru na jinsi  ambapo Pango la kuzaliwa kwa Bwana, na  mti kwa mwaka huu vinatoka katika maeneo mawili ya mbali kijiografia,  lakini yanayofanana, kwa upande wa milima, ambapo jumuiya huhifadhi hai wa tangazo la malaika na Noeli huhifadhi uzuri wake  na maana yake ya kina. Alielezea pango na baadhi ya wahusika wake na mti wa Noeli huku akisisitiza juu ya mapambo yaliyofanywa kwa ustadi mkubwa na mawazo na vijana na wazee pamoja. Kwa maana hiyo alisema kwamba upendo uweze kuchukua nafasi dhidi ya vurugu na  kuwaalika  kila mtu kupeleka habari njema ya kuzaliwa kwa Bwana kila mahali. Na wakati wa  kutoa neno kutoka kwa wajumbe, wa kwanza alikuwa ni Bwana Mario Bùcaro Flores, Waziri wa Mahusiano ya Kigeni wa Guatemala ambaye alisema: kujivunia fursa ya kufanya sanaa ya nchi yake kujulikana duniani kote kwa njia ya Kuzaliwa kwa Kristo iliyotolewa kwa Papa Francisko, zawadi ambayo pia inadhihirisha umakini wa Guatemala katika uhuru wa kidini na kujitolea kwake kwa amani.

Pango na Mti wa mapambo ya Siku Kuu ya Noeli mjini Vatican
Pango na Mti wa mapambo ya Siku Kuu ya Noeli mjini Vatican

Kwa niaba ya Askofu Mkuu wa Udine, Padre Harry Della Pietra alikuwa na ya kusema na kukumbuka  umuhimu wa pango ambao unakumbusha  fumbo la Umwilisho wa Mwana wa Mungu. Yesu alijifanya mdogo, kwa kunukuu maneno ya Papa Francisko aliyokuwa amewaeleza wakati wa mkutano wao kuwa ili kukutana na Mungu sisi pia lazima tujifanye wadogo na kuwa watu walio karibu na wengine. Kwa upade wa Bwana  Massimo Fedriga, Mkuu wa Mkoa wa Friuli-Venezia Giulia, eneo ambalo limetengeneza Pango  alisema  ni ishara ya ushirikiano wa jumuiya nzima yenye uthabiti ambayo imeteseka na kuweza kuzaliwa upya mara nyingi. Alitaja tetemeko la ardhi, janga ambalo lilikumba sana Friuli-Venezia Giulia na dhoruba ya Viara iliyoharibu misitu na misitu miaka minne iliyopita. Ili kufanya tukio hilo la kuzaliwa kwa Yesu, alisema, vipande vilivyobaki wakati wa dhoruba vilipatina na  mzizi iliong'olewa kutoka katika ardhi ya watu wenyewe ambapo vyote hivyo vimekuwa chimbuko la pango la Kuzaliwa kwa Yesu. Hatimaye, Meya wa Sutrio, Mattia Manlio, alijikita kuelezea juu ya  mila  na utamaduni mkuu wa kazi ya mbao ambayo jumuiya yake imeweza kudumisha uhai wake  bila kupoteza utajiri wa uzoefu uliotolewa kutoka kwa vizazi vilivyotangulia.

Kwa upande wa ujumbe kutoka katika eneo la Rosello: askofu Claudio Palumbo, wa jimbo la Trivento, alitaja maneno mawili: mizizi na tafakari. Ya kwanza alisema kifungo na dunia, ya pili, kwa kutafakari pango, linazungumza juu ya mbingu, mambo yote mawili yalifanywa kuwa moja ndani ya Yesu. Hali mbili zinazorutubisha kila mmoja na zinaonesha maana kamili ya maisha ambayo ulimwengu unahitaji sana leo hii. Na Meya wa Rosello, Alessio Monaco, alisisitiza shughuli ya kwaya iliyohusisha watoto wa taasisi, wageni wa wazee wa nyumba ya wazee na wanafunzi wa baadhi ya shule kwa ajili ya uundaji wa mapambo ya mti wa Noeli, uliopambwa katika uwanja wa Mtakatifu Petro, ni  fursa kubwa ya kujumuishwa alisema na ambayo inaonesha hisia changamfu ya jumuiya ambayo mtu anapumua katika vijiji vya Abruzzo.

Pango na Mti wa mapambo ya Siku Kuu ya Noeli mjini Vatican
Pango na Mti wa mapambo ya Siku Kuu ya Noeli mjini Vatican

Katika Ukumbi wa Paulo VI,  naye Sr.  Raffaella Petrini alikuwa na shughuli ya kuhitimisha. Katika hotuba yake alikumbuka umuhimu ambao Noeli kwa upandewa  Mtakatifu Francis wa Assisi, ambaye alikuwa anauona kama  sikukuu ya siku kuu na kwa Mtakatifu Clara. Ni ushuhuda wa upendo wa Mungu kwa wanadamu, wakati mti unawakilisha uzima wa milele na tumaini la Ufufuko. Akinukuu kile  ambacho Papa Francisko alisema kwa mahujaji kutoka Bavaria ambao walitoa misonobari mwaka wa 2013 alisema “ Wakati wa Noeli, tangazo la furaha la malaika kwa wachungaji wa Bethlehemu linasikika kila mahali: (...) Injili Inasema Wachungaji hao  walifunikwa na nuru kuu. Kwa maana hiyo hata leo, Yesu anaendelea kuondoa giza la makosa na dhambi, ili kuwaletea wanadamu furaha ya nuru ya kimungu yenye kung’aa, ambayo mti wa Noeli  ni ishara na ukumbusho wake. Hebu tujiruhusu sisi wenyewe kufunikwa na nuru ya ukweli wake”. Kwa maana hiyo Sr Petrini alirudia kusema “Hebu pia tujiruhusu sisi wenyewe kufunikwa,kwa mwanga wa Noeli na tutumaini kwamba katika wakati huu hisia ya kuzaliwa upya na hamu ya udugu itaaambatana nasi.

Uzindizi wa Pango na Mti mrefu wa Mapambo ya siku kuu ya Noeli 2022
04 December 2022, 15:26