Tafuta

2024.07.09 Kardinali Pietro Parolin,Katibu wa Vatican. 2024.07.09 Kardinali Pietro Parolin,Katibu wa Vatican.  (Daniele Scudieri - Imagoeconomica)

Kard.Parolin,Kyiv,Odessa-Ukraine na mikutano na mamlaka ya raia na kidini

Katibu wa wa Vatican kuanzi tarehe 19 hadi 24 Julai 2024 atakuwa katika nchi ya Ulaya Mashariki.Ni ziara ya kwanza tangu mwanzo wa uchokozi wa Urusi.Kardinali Parolin ataongoza Misa katika Madhabahu ya Maria wa Berdychiv kwa ajili ya maadhimisho ya mwisho ya hija ya Wakatoliki wa Ukraine wa ibada ya Kilatini.

Vatican News

Kuanzia tarehe 19 Julai 2024, Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican  ameanza safari ya kwenda iliyoteuliwa na Papa kama Mwakilishi wake kwa ajili ya maadhimisho ya mwisho ya hija ya Wakatoliki wa Ukraine wa ibada ya Kilatini, ambayo itafanyika mwezi Julai katika Madhabahu ya Maria wa  Berdychiv. Hii ni ziara kwanza katika nchi ya Ulaya Mashariki tangu kuanza kwa uvamizi wa Urusi, na ambayo itakamilika tarehe 24 Julai 2024.

Akaunti ya X

Kupitia Akaunti ya X @TerzaLoggia ilitangaza kuwa: “Siku hizi kuna ahadi na mipango mbalimbali iliyoratibiwa, ataacha katika Kyiv na Odessa na kukutana na mamlaka ya kiraia na kidini. Kardinali ataongoza Misa katika Madhabahu ya Maria  ya Berdychiv kwa ajili ya maadhimisho ya mwisho ya hija ya Wakatoliki wa Ukraine wa ibada ya Kilatini.”

Misa katika Madhabahu ya Berdychiv

Kardinali Parolin hata hivyo atatumia muda mfupi tarehe 19 Julai 2024  katika Uaskofu Mkuu wa Lviv ya Kilatini, kisha atatembelea jiji la Odessa. Dominika tarehe 21 Julai, Kardinali Parolin ataongoza Misa huko Berdychiv kwa ajili ya maadhimisho ya mwisho ya hija ya Wakatoliki wa Ukraine. Madhabahu hiyo iko katika mkoa wa Zhytomyr (jimbo), magharibi mwa Kyiv, na ni marudio ya mahujaji ambayo huleta pamoja waamini wa Kikatoliki kutoka Ukraine na pia kutoka nchi zingine. Katika miaka hii miwili ya mwisho mahujaji wanakwenda huko kuomba hasa maombezi ya Maria kwa ajili ya amani.

Mkutano na mamlaka

Katika siku chache zijazo Kardinali Parolin atatembelea Kanisa Kuu la Kigiriki la Kikatoliki la Kyiv. Mkutano na Askofu mkuu wa Kanisa Katoliki la Kigiriki la Kiukreni, Sviatoslav Shevchuk. Pia katika mpango huo ni mkutano wa Katibu wa Vatican na mamlaka ya kiraia na kidini ya nchi.

Kardinali Parolin yuko Ukraine kuanzaia 19 hadi 24 Julai 2024
19 July 2024, 16:15