Tafuta

Mwaka mmoja wa WYD,Lisbon 2023:picha na maneno ya mkutano na Yesu hai

Baada ya mwaka mmoja tangu kufanyika Siku ya Vijana Duniani huko Lisbon nchini Ureno mnamo mwaka 2023,Baraza la Kipapa la Walei,Familia na Maisha,limechapisha tarehe 6 Agosti 2024,video ya picha na maneno ya Papa Francisko na mkutano na Yesu aliye hai.

Vatican News

Sauti ya Baba Mtakatifu ikiwasihi washiriki milioni moja na nusu wasiogope yajayo, nyuso za mahujaji waliokuja Lisbon kutoka pande zote za dunia na muziki wa wimbo "Ai pressa no ar": ndivyo viungo vya video iliyochapishwa tarehe 6 Agosti 2024  kwenye Tovuti  rasmi ya Baraza la Kipapa la Walei, Familia na Maisha  kuhusu Siku ya Vijana Duniani,  katika kuadhimisha kumbukumbu ya mwaka mmoja  wa Siku hiyo iliyomalizika tarehe 6 Agosti 2023   huko Lisbon nchini  Ureno.

Kardinali Aguiar:Ilistahili,kwa sababu tulikuwa Kanisa lililo hai la Bwana Wetu

Akitoa maoni yake Mratibu Mkuu wa Siku ya Vijana Duniani ya Ureno(WYD), Mwadhama Kardinali Americo Manuel Alves Aguiar, alisema kuwa “Mwaka mmoja baadaye ninatazama nyuma na ilikuwa na thamani yake. Kila siku, kila safari, kila mkutano tena na kumekuwa na maelfu  ya  kila sherehe.

WYD 2023 Lisbon Ureno
WYD 2023 Lisbon Ureno

Mwaka mmoja baadaye, kama kawaida mwishoni mwa kila Siku ya Vijana Ulimwenguni, hakuna mtu anayeweza kufikiria matunda yanayoweza kuzaliwa na kukua katika maisha ya mahujaji vijana, Makanisa mahalia au hata Kanisa la Ulimwengu. Hatuna uwezo wa kufanya hesabu kama hizo tunapozungumza juu ya maisha ya Mungu katika moyo wa mwanadamu. Hata hivyo, hatua kwa hatua, katika maisha ya kawaida ya Kanisa, Mungu anafanya kazi kubadilisha maisha ya kila mtu.

Siku ambazo haziwezi kusahulika
Siku ambazo haziwezi kusahulika

 Kardinali Aguiar, aliendelea kueleza kuwa: “Ilistahili, zaidi ya yote, kwa sababu tulikuwa Kanisa lililo hai la Bwana Wetu  na ambaya huimba, kuomba na kulia. Ambaye anafurahi, huzuni, amejaa tumaini na uaminifu. Anayeungana tena ndani ya Yesu na Yesu aliye hai.” Ambao hukusanyika karibu na Mchungaji na kufurahi tu kumwona akipita. Kanisa lililo hai la Bwana Wetu, ambapo sisi sote ni wana na binti wapendwa, wote, wote, wote.”

Novemba,alama za WYD kutoka Lisbon kwenda Seoul-Korea Kusini

Sasa, kwa jicho la kuelekea Seoul 2027, kuvuka Jubilei ya Vijana mwaka 2025 ambapo Baraza la Kipapa la Walei, Familia na Maisha linaendelea kusindikiza  na maandalizi ya Siku ya Vijana duniani inayokuja kwa kiwango cha Makanisa mahalia, ambayo itaadhimishwa kwenye Maadhimisho ya Kristo Mfalme, Dominika  tarehe 24 Novemba 2024. Katika tukio hilo, alama za mkutano zitapitishwa na kukabidhiwa ambazo ni  msalaba na nakala ya Picha  ya Maria ya Salus Populi Romani (Maria Afya ya Waroma) kutoka kwa vijana wa Lisbon kuelekea kwa vijana wa Seoul.

Mkutano na wakujitolea Lison 2023
Mkutano na wakujitolea Lison 2023
Video ya WYD 2023 imechapishwa
07 August 2024, 16:25