Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Récitatif et Scherzetto
Ratiba Podcast
Janga la utumwa halikutokea katika siku za nyuma tu:kwa bahati mbaya linaendelea kutokea hata leo na katika nchi kadhaa. Janga la utumwa halikutokea katika siku za nyuma tu:kwa bahati mbaya linaendelea kutokea hata leo na katika nchi kadhaa. 

Vatican:Lazima Kutokomeza Utumwa wowote ule kwa njia ya Elimu!

Katika hotuba ya Monsinyo Juan Antonio Cruz Serrano anabainisha juu ya kukuza na kutetea uhuru na haki ya kijamii kwa kuongeza ufahamu ndani ya jamii,kuanzisha uratibu bora kati ya serikali, mamlaka ya mahakama na sheria na wafanyakazi wa kijamii.Amefafanua hayo katika fursa ya kumbukizi ya Siku ya Kimataifa ya Kuadhimisha Waathiriwa wa Utumwa na Biashara ya Utumwa ya Bahari ya Altlantiki,iadhimishwayo kila mwaka mnamo Machi 25.

Na Angella Rwezaula – Vatican.

Monsinyo Juan Antonio Cruz Serrano, Mwakilishi wa  kudumu wa Vatican katika Baraza la Umoja wa Mataifa la Marekani (OAS), alizungumza tarehe 25 Machi 2025 mjini Washington katika kikao maalum cha Baraza la Kudumu la Shirika katika kukumbuka waathirika wa utumwa na biashara ya watumwa kupitia bahari ya Atlantiki (Transatlantic,) inayoadhimishwa na Umoja wa Mataifa kila mwaka Machi 25. Tukio hilo liliambatana na Juma la  VIII ya Wamarekani Wenye Asili ya Kiafrika na elimu ya kijamii ya utumwa katika Bara  ka Amerika.

Janga la utumwa mamboleo

Mwakilishi wa kudumu alibainisha kwa uchungu kwamba janga la utumwa halikutokea katika siku za nyuma tu: kwa bahati mbaya linaendelea kutokea hata leo na katika nchi kadhaa. Ikiwa tutafumba macho na masikio yetu kwa jambo hili, tutakuwa tukishirik" ndani yake, aliongeza, akinukuu maonyo ya Papa juu ya suala hilo. Utumwa unamlenga  mwanadamu, ambaye thamani yake imepunguzwa kuwa ya manufaa kwa mtu au kitu, Papa Francisko  alikuwa amesisitiza hayo mwaka  2023 na, hata mapema katika waraka wa  Fratelli Tutti wa 2020, yaani Wote ni ndugu  na alikuwa ametuhimiza kukumbuka daima bila kuchoka na bila kujiumiza sisi wenyewe, mateso, biashara ya utumwa na makabila mengi ya leo.

Juhudi za kuondoa utumwa kwa bidii ya elimu

Juhudi za kuondoa utumwa mambo leo , pamoja na majanga mengine mengi ya ulimwengu wa kisasa, zinapaswa kuwa kwa umoja, katika muktadha mpana wa wasiwasi wa kuanzisha michakato" inayoongoza amani yenye upatanisho muhimu kati ya watu, ambapo utambuzi wa hadhi ya mwanadamu unachukua nafasi kuu. Elimu na mafunzo, katika kuendeleza dhamira yake kupitia taasisi zake za kuhakikisha hali ya kutosha ya elimu na mafunzo kwa hiyo inalenga katika elimu ya maadili, kijamii na kiroho yenye uwezo wa kujumuisha uzoefu mpya na tofauti wa sekta hizo za jamii ambazo mara nyingi zimefanywa zisizoonekana na kunyamazishwa, kama ilivyo kwa waathiriwa wa biashara haramu ya binadamu. Kwa kumalizia, ujumbe wa Vatican  uliwashukuru wale waliohudhuria kwa hisia za ukaribu zilizooneshwa kwa Papa, hata wakati wa kulazwa hospitalini.

27 Machi 2025, 16:14
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031