Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
PROGRAMU YA KISWAHILI
Ratiba Podcast
2025.04.04 Uwasilishaji wa Jubilei ya Wagonjwa. 2025.04.04 Uwasilishaji wa Jubilei ya Wagonjwa. 

Jubilei ya wagonjwa Aprili 5-6:Shuhuda hai wakati wa ugonjwa!

Jubilei ya Wagonjwa na Ulimwengu wa Afya iliwasilishwa tarehe 4 Aprili 2025 kwa waandishi wa habari ambayo imeanza tarehe 5 Aprili na itahitimishwa Aprili 6 kwa ibada ya misa Takatifu.Shuhuda mbali mbali na mifano kwa anayeishi na ugonjwa akiwa na Mungu karibu zilisikika.

Vatican News

Katika ofisi ya waandishi wa habari mjini Vatica Ijumaa tarehe 4 Aprili 2025 iliwasilishwa baadhi ya shuhuda za madaktari na wasio, ambao ni wahusika wakuu  katika tukio la kuishi Jubilei ya Wagonjwa na Ulimwengu wa kiafya, (5-6 Aprili 2025),mojawapo ya tukio kuu  la Saba kwa  Mwaka Mtakatifu, kama ilivyopangwa katika ratiba ya matukio makuu ya Jubilei. Miongoni mwa washiriki katika hatua ya mkutano huo, alikuwa  Monsinyo Graham Bell, Katibu Msaidizi anayesimamia wa Baraza la Kipapa Uinjilishaji, Sehemu ya Masuala Msingi ya Uinjilishaji Ulimwenguni, na Dk. Lucia Celesti, Daktari katika Hospitali ya Kipapa ya Watoto Bambino Gesù, anayehusika na Mapokezi, ambaye alizungumza juu ya dhamira ya hospitali hiyo katika Jubilei hii yam waka Mtakatifu 2025.

"Tumaini ni sehemu ya DNA yetu. Watoto kutoka maeneo ya vita daima wamefika hospitalini, lakini na tunakuwa karibu sana pia ni wengi kama katika miaka ya hivi karibuni. Kukaribisha familia ambayo nyumba yao ilipigwa kwa bomu na ambayo inaweza kuhifadhi chuki ya kizazi kwa wale ambao walipiga nyumba zao, na kuwakaribisha kwa upendo, kiukweli inasaidia kuvunja mzunguko ambao ungekuwa na matokeo ya upendo ambayo yangekuwa na uwezo wa kusambaza baadaye."

Ukiona vifo vingi lazima uogope ila imani ni muhimu

Dk. Rocìo Bellido Octavio ni muuguzi katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Jorge cha Zaragoza na amekuwa na shughuli nyingi wakati wa janga hili alisema: “Unapoona vifo vingi, unapoona hali mbaya, unaona kwamba hudhibiti ugonjwa huo na kwamba hujui, unaogopa, lakini katika muktadha huu imani ni muhimu ili kufanya kazi kwa uhakika kwamba Mungu alikuwa pamoja nami. Imani, haikunisaidia kuelewa hali hiyo, ilinisaidia kuisimamia, kupata nguvu nilipokuwa sina iliyobaki, kuvuta pumzi nilipohisi kwamba ninaikosa,”alisisitiza.

Ushuhuda wa mwenyeheri Benedetta Bianchi Porro

Kwa upnde wa Padre Andrea Vena, Afisa wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano na msimamizi wa Mchakato wa Kutangazwa Mtakatifu, Benedetta Bianchi Porro, alisimulia historia ya Mwenyeheri Benedetta Bianchi Porro kuwa: "Benedetta alifariki akiwa mchanga, historia yake ni ya sasa, ya kisasa, historia iliyooneshwa na machafuko makubwa. Mwishowe atabaki kuwa kiziwi, kipofu, amepooza na bado anaimba maisha, furaha, kukubali hali yake na kuikumbatia kikamilifu."

05 Aprili 2025, 13:37
Prev
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930   
Next
May 2025
SuMoTuWeThFrSa
    123
45678910
11121314151617
18192021222324
25262728293031