Tafuta

Cookie Policy
The portal Vatican News uses technical or similar cookies to make navigation easier and guarantee the use of the services. Furthermore, technical and analysis cookies from third parties may be used. If you want to know more click here. By closing this banner you consent to the use of cookies.
I AGREE
Balletto completo
Ratiba Podcast
Trump na Putin Trump na Putin  (AFP or licensors)

Ukraine,kuelekea mazungumzo mapya kati ya Trump na Putin

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuwa atazungumza na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin Jumanne,Machi 18,kuhusu pendekezo la kusitisha mapigano kwa siku 30 lililosimamiwa na Marekani na kukubaliwa na Ukraine mnamo Machi 11.

Na angella Rwezaula – Vatican.

Rais wa Marekani Donald Trump aliwaambia waandishi wa habari ndani ya ndege ya (Air Force One) alipokuwa akirejea Washington kutoka Florida kuwa: "Nitazungumza na Rais Putin Jumanne(kwa maana ya tarehe 18 Machi 2025). Tulifanya kazi kwa bidii mwishoni mwa juma." Trump aliongeza kusema kuwa “kuna uwezekano mkubwa kwamba mazungumzo na Putin yatakuwa na matokeo chanya.” Wakati wa mkutano huo, Trump alisema, watazungumza pia kuhusu maeneo na mitambo ya nishati. Naye Mjumbe maalum wa Marekani Steve Witkoff alisema Dominika 16 Machi 2025 kwamba,  Trump na Putin watakuwa na "majadiliano ya kuvutia na chanya ndani ya Juma."

Moscow,Kyiv na Washington zinataka vita imalizike

Moscow, Kyiv na Washington "zinataka hii imalizike," mwanadiplomasia huyo aliongeza kwa shirika la Ahabari la (CNN). Bado haijafahamika ni masharti gani yatapelekea Urusi kuidhinisha usitishaji huo. Kwa mujibu wa ripoti za hivi karibuni, zinaeleza kuwa Kyiv huenda ikalazimika kujinyima uanachama wake na NATO na kukubali kuachia maeneo yanayokaliwa kwa sasa na majeshi ya Moscow.

Kyiv Inabadilisha Uongozi wa Kijeshi, Kombora jipya lilijaribiwa

Wakati mazungumzo ya mapatano kati ya Urusi na Ukraine yakiendelea, Zelensky alitangaza mjini Kyiv kwamba wanajeshi wa Ukraine wamefanyia majaribio kombora jipya la masafa marefu lenye uwezo wa kuchukua umbali wa kilomita 1,000. Kwa hiyo, Long Neptune inayozalishwa nchini ingeweza kufika Moscow. Vyanzo kadhaa visivyo rasmi vinaripoti kwamba shambulio la Ijumaa kwenye kiwanda cha kusafisha mafuta cha Tuapse katika eneo la Krasnodar la Urusi lilitekelezwa kwa kombora hilo jipya. Wakati huo huo, Zelensky mwenyewe alitangaza mabadiliko mapya juu ya Kikosi cha Wanajeshi, akimbadilisha Mkuu wa Wafanyakazi Anatoly Barhylevych na Meja Jenerali Andriy Gnatov. Uamuzi huo ungejibu hitaji la kuongeza "ufanisi wa usimamizi wa wima wa vikosi vya jeshi", kulingana na rais wa Ukraine.

Ukraine yaangusha ndege 90 kati ya 174

Jeshi la Ukraine lilitangaza kuwa limeangusha ndege 90 kati ya 174 zilizorushwa na Urusi usiku kucha. Vikosi vya Urusi, kwa upande wao, vilisema viliharibu ndege 72 za Ukraine zilizolenga maeneo kadhaa ya Urusi, pamoja na Kursk. Pia usiku kucha, vikosi vya Ukraine vilifanya shambulio kubwa la ndege zisizo na rubani kwenye vituo kadhaa vya miundombinu, pamoja na eneo kubwa la mafuta na nishati, katika mkoa wa Astrakhan nchini Urusi. Shambulio hilo - linaripoti shirika la habari la Urusi Tass - lilisababisha moto, mtu mmoja alijeruhiwa na mitambo ambayo wafanyikazi walikuwa wamehamishwa.

17 Machi 2025, 15:00
Prev
March 2025
SuMoTuWeThFrSa
      1
2345678
9101112131415
16171819202122
23242526272829
3031     
Next
April 2025
SuMoTuWeThFrSa
  12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
27282930